Rais mstaafu wa awamu ya Nne, Dkt.
Jakaya Mrisho Kikwete, (kushoto), akisalimiana na Waziri Mkuu (mstaafu)
ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Mhe. Edward Lowassa,
wakati akimpokea nyumbani kwake Msasani kwenye msiba wa baba mkwe wake
leo Ijumaa Julai 20, 2018. Wawili hao wanao urafiki wa muda mrefu ambao
mara kadhaa wamewahi kuutangaza hadharani.
Mama
Salma Rashid Kikwete Mke wa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, amefiwa na Baba yake
Mzazi Mzee Rashid Mkwachu. Na mazishi yalitarajiwa kufanyika Alasiri hii kwenye
makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam.
No comments :
Post a Comment