Monday, June 11, 2018

PWANI ,DAR NA RUVUMA WAFUNZWA MATUMIZI YA MIFUMO YA EPICOR


EPICOR 10 MTWARA (1)
Msimamizi wa Fedha Tamisemi Bi Ummy Wayayu(kushoto) akijadili jambo mara baada ya ufunguzi wa mafunzo ya siku nne ya  Mfumo wa usimamizi wa fedha za umma (Epicor 10.2) yanayoendelea yaliyoanza mkoani mtwara na kushirikisha wahasibu,waweka hazina na maafisa usimamizi wa fedha wa mikoa ya Pwani,Mtwara, kinondoni manispaa na Ruvuma…Katikati ni Hafidh Issa,Mweka hazina Kisarawe na Suzan Chaula Mweka hazina Halmashauri ya mji wa Kibaha Mkoani Pwani
EPICOR 10 MTWARA (7)
Kiongozi wa timu ya mifumo ya fedha katika mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma PS3, Dokta Gemini Mtei, akitoa somo kwa washiriki wa mafunzo ya matumizi ya mfumo wa usimamizi wa fedha za umma (EPICOR 10.2), yanayoendelea mkoani Mtwara yakishirikisha wahasibu na waweka hazina wa halmashauri za mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Mtwara na Ruvuma. Mafunzo ambayo yanaendeshwa na Ofisi ya Rais TAMISEMI chini ya mradi wa PS3 unaofadhiliwa na shirika la Kimarekani la USAID.
EPICOR 10 MTWARA (5)
Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya matumizi ya mfumo wa usimamizi wa fedha za umma (EPICOR 10.2), yanayoendelea mkoani Mtwara yakishirikisha wahasibu na waweka hazina wa halmashauri za mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Mtwara na Ruvuma, wakifuatilia somo. Mafunzo ambayo yanaendeshwa na Ofisi ya Rais TAMISEMI chini ya mradi wa PS3 unaofadhiliwa na shirika la Kimarekani la USAID.
EPICOR 10 MTWARA (6)
 Mhasibu wa manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, Pendo Sangija (kushoto) na Mweka hazina wa halmashauri ya mji wa Nanyamba mkoani Mtwara, wakifuatilia somo kutoka kwa wawezeshaji wa mafunzo ya matumizi ya mfumo wa usimamizi wa fedha za umma (EPICOR 10.2), yanayoendelea mkoani Mtwara yakishirikisha wahasibu na waweka hazina wa halmashauri za mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Mtwara na Ruvuma. Mafunzo ambayo yanaendeshwa na Ofisi ya Rais TAMISEMI chini ya mradi wa PS3 unaofadhiliwa na shirika la Kimarekani la USAID.
………………..
Na ABDULAZIZ AHMEID -MTWARA
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwa kushirikiana naMradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3) wanaendelea natoa mafunzo ya kina kwa
watumishi wa kada  ya uhasibu kutoka  mamlaka  185  za Serikali za Mitaa Tanzania.
Akifungua mafunzo hayo yanayohusu mfumo  mpya wa Epicor 10.2, leo  katika manispaa ya Mtwara ,Afisa msimamizi wa mifumo ya fedha Tamisemi,Bi Ummy Wayayu amesema mafunzo hayo ya mfumo wa Epicor yamelenga kuwapa uelewa Wahasibu juu ya mabadiliko ya maboresho makubwa yaliyofanywa katika mfumo huo.
Mafunzo hayo yanaendeshwa kutokana na  Halmashauri nchini kuanza matumizi ya mfumo katika toleo lililojulikana kama Platnum mwaka 1999/2000 na baadaye mfumo ulifanyiwa maboresho na kufungwa epicor toleo Na 7.2 mwaka 2001 wakati huo mfumo ukiwa umefungwa katika Halmashauri 38 pekee
Na ilipofika  mwaka 2014/15 mfumo uliboreshwa na kuwa epicor toleo la 7.3.5 na kufungwa katika Halmashauri 44 zaidi hivyo kuwa na Jumla ya Halmashauri 82zilizokuwa zinatumia mfumo na hadi kufikia july Mwaka 2012, TAMISEMI ilifanya maboresho makubwa kwa kuunganisha Halmashauri  133 zilizokuwepo wakati huo kupitia  kampuni ya simu ya taifa TTCL na kuweka epicor toleo namba 9.05 ambalo limeendelea kutumika hadi sasa.
Hata hivyo Halmashauri zilizoongezeka baadaye zilifungwa epicor toleo namba 10.1 ambalo limeboreshwa sasa na kuwa 10.2 inayofungwa Halmashauri zote zimeanza matumizi ya epicor toleo namba 10.2 ambayo ni hatua kubwa sana katika utekelezaji wa dhana nzima ya uwazi uwajibikaji na utawala bora katika usimamizi wa fedha za umma.
Kwa upande wao baadhi ya washiriki akiwemo mweka hazina wa Halmashauri ya Bagamoyo,kibaaha na kisarawe mkoani Pwani walibainisha kuwa mfumo huo utasaidia Halmashauri kuondokana na vyeti vya hati chafu na zile zenye mashaka kutokana na mapato na matumizi ya fedha zote kutakiwa kuingizwa katika mfumo huo.
Aidha walibainisha kuwa uboreshaji wa mfumo wa Epicor ni muendelezo wa uboreshaji wa mifumo ya Serikali kama ilivyofanyika kwa mifumo mingine kama vile mifumo ya Afya. 
Maboresho mengine yaliyofanyika katika mfumo huo wa Epicor 10.2  ni kwamba mifumo yote ya msingi ya usimamizi wa fedha katika sekta za umma kwa sasa itaweza kuwasiliana na kushirikishana taarifa ambapo hapo awali, uongozi na maafisa katika Mamlaka za Serikali za Mitaa walilazimika kupitia mipango na bajeti katika mfumo mmoja, mapato katika mfumo mwingine na matumizi kwenye mfumo mwingine, hivyo kuleta ugumu katika kudhihirisha uwajibikaji, ufanisi na thamani ya fedha katika matumizi ya fedha za Serikali.
Sambamba na kutumika kwa mfumo huo ambao  utaunganishwa na mfumo unaowezesha mabenki kulipana Tanzania (TISS) ambao utaruhusu malipo yote kufanyika kwa njia ya kielektroniki. 
Mafunzo hayo yanafanyika katika vituo sita  ambavyo ni Dodoma,Mwanza, Mtwara, Iringa, Kagera na Mbeya yakijumuisha watumiaji wa mfumo huo ambao ni Waweka Hazina na Wahasibu na baadaye Maafisa TEHAMA, Maafisa Manunuzi na Wakaguzi wa Ndani na kuendeshwa na PS 3 kwa usimamizi wa Tamisemi na kufadhiliwa na USAID
Washiriki waliopewa mafunzo kupitia kituo cha kanda ya mtwara ni pamoja na mikoa ya Lindi,Mtwara,Ruvuma na sasa ni Pwani Dar es sallam na baadhi ya wilaya za mkoa wa mtwara

No comments :

Post a Comment