Wednesday, May 9, 2018

Msajili Baraza la Uuguzi Tanzania Aanza Kazi Rasmi


001
Msajili wa Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania, Bi. Agnes Mtawa akikaribishwa leo ofisini na watumishi wa baraza hilo. Kushoto ni Bi. Jane Mazigo aliyekuwa akikaimu nafasi hiyo akimpatia maua Bi. Agnes Mtawa na kulia ni Happy Masenga anayeshughulika na mafunzo katika baraza hilo.
002
Bi. Mtawa akitazama zawadi ya maua aliyokabidhiwa na watumishi wa baraza hilo leo.
003
Msajili akiwa katika picha pamoja na watumishi wa baraza hilo leo. Kutoka kushoto ni Bi. Jane Mazigo na Bi. Happy Masenga.
……………………..
Msajili wa Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania, Bi. Agnes Mtawa leo ameanza kazi rasmi baada ya kukabidhiwa ofisi tangu alipoteuliwa kushika nafasi hiyo mwezi uliopita. Bi. Agnes Mtawa anachukua nafasi ya Bi. Lena Mfalila aliyemaliza muda wake.

Awali Bi. Mtawa alikuwa Mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) ambapo mwezi uliopita Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu alimteua kuwa Msajili wa Baraza la Uuguzi Tanzania.
Uteuzi huo ulianza rasmi tarehe 16-04-2018 na kwamba utadumu kwa muda wa miaka mitano kuanzia tarehe ya uteuzi.
Nafasi mbalimbali alizowahi kushika katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Bi. Mtawa ni; Mkuu wa Mafunzo na Uajiri kuanzia mwaka 2004 hadi 2006, Mkuu wa Mafunzo, Utafiti na Elimu kuanzia mwaka 1997 hadi 2004, amewahi kuwa  Katibu Mkuu katika baraza la uuguzi na ukunga Tanzania kuanzia 2002  hadi 2011 na mwaka 2007 aliteuliwa Mkuurugenzi wa Uuguzi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili hadi mwezi uliopita alipoteuliwa.

No comments :

Post a Comment