Wednesday, May 9, 2018

Mfumo Wa Kielektroniki Kuchochea Ukuaji wa Biashara

????????????????????????????????????
  Katibu Tawala Msaidizi Sekta za Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Dodoma  Bibi  Aziza Mumbi akizungumza na waandishi  wa Habari (hawapo pichani) kuhusu faida za  mfumo wa Kusajili Kampuni kwa njia ya mtandao leo Jijini Dodoma.
????????????????????????????????????
Meneja Uboreshaji Mazingira ya Biashara na Uwekezaji kutoka Baraza la Taifa la Biashara Bw.  Willy Magehema akizungumza  wakati wa  ufunguzi wa mafunzo ya siku mbili kwa maafisa Biashara na TEHAMA wa Wilaya zote za Mkoa wa Dodoma.
????????????????????????????????????
Sehemu ya Washiri wa Mafunzo hayo wakifuatilia  hotuba ya mgeni rasmi wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya mfumo wa Kusajili Kampuni kwa njia ya mtandao leo Jijini Dodoma
????????????????????????????????????
Katibu Tawala Msaidizi Sekta za Uchumi na Uzalishaji Bibi  Aziza Mumbi akiwa kwenye picha ya pamoja na Washiri wa Mafunzo ya mfumo wa Kusajili Kampuni kwa njia ya mtandao leo Jijini Dodoma.
????????????????????????????????????
Msajili  Mwandamizi  kutoka BRELA  Bw. Lumambo Shiwala akisisitiza kuhusu umuhimu wa mfumo huo katika kukuza biashara.
( Picha zote  na  MAELEZO
………………
Na Mwandishi Wetu
Serikali imeanzisha Mfumo wa Kielektroniki utakaotumika kusajili Makampuni, Majina ya Biashara,Leseni za Viwanda, hati, Alama za biashara na huduma  Kote nchini.
Akizungumza wakati akifungua Mafunzo ya siku mbili kwa Maafisa Biashara wa Wilaya zote za Mkoa wa Dodoma Katibu  Tawala Msaidizi  Mkoa wa Dodoma anayeshughulikia Uchumi na
Uzalishaji Bibi Aziza Mumba amesema kuwa mfumo huo utaongeza tija kwa  wajasiriamali na wafanyabiashara  wanaohitaji leseni za Biashara kupitia mfumo huo wa kielektroniki.
Akizungumzia Mfumo huo Bibi Mumba amesema  umeanza kutumika kwa awamu ya kwanza kuanzia tarehe 4 Januari , 2018 kwa kusajili alama za Biashara kwa njia ya mtandao ambapo mfumo huo umeacha madirisha wazi kwa ajili ya kuweza kuunganisha na mifumo ya Taasisi nyingine za Serikali zitakapokuwa tayari.
“Natoa shukrani za Dhati kwa mradi wa uboreshaji mazingira ya Biashara kwa kuwezesha ujenzi wa vituo vya biashara kwa Wilaya zote za Mkoa wa Dodoma hali itakayowezesha wafanyabiashara kupata huduma zote katika eneo moja” Alisisitiza Bibi Mumba
Alifafanua kuwa kwa kuzingatia umuhimu wa mfumo huo BRELA kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Biashara  (TNBC) wameandaa mafunzo kwa watendaji wa vituo hivyo ili kuwawezesha kutoa huduma kwa wafanyabiashara na wawekezaji watakaohitaji msaada wa ziada katika kutumia mfumo huo katika kusajili makampuni kwa njia ya mtandao.
Aliongeza kuwa washiriki wa mafunzo hayo ambao ni Maafisa  Biashar na Maafisa TEHAMA   wana wajibu wa kutoa elimu ya mfumo huo kwa wananchi wote kupitia Mabaraza ya Madiwani ya Halmashauri na Mabaraza ya Maendeleo ya Kata.
Kwa upande wake Meneja Uboreshaji Biashara na uwekezaji wa Baraza la Taifa la Biashara (TNBC) amesema kuwa ili kujisajili na kupata huduma zote katika mfumo huo wa TEHAMA lazima mwombaji awe na kitambulisho cha Taifa.
Aliongeza kuwa mfumo huo utasaidia kuongeza tija katika kusajili biashara na kusaidia urasimishaji wa Biashara hali itakayochochea kukua kwa biashara hapa nchini.
 Urasimishaji biashara ni hali kuifanya biashara kutambulika kisheria kwa kuzingatia sheria, Kanuni na taratibu zilizopo ambapo utoaji wa leseni za Biashara unasimamiwa na sheria ya leseni za Biashara Na. 25 ya mwaka 1972 pamoja na marekebisho yak echini ya sheria NA. 9 ya mwaka 1980.
Mfumo huu umeunganishwa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) kwa ajili ya namba za utambulisho wa Taifa, Mamlaka ya mapato Tanzania  (TRA) kwa ajili ya kutoa Namba ya Utambulisho kwa mlipa kodi (TIN)  na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa ajili ya utambuzi wa maeneo nchini.

No comments :

Post a Comment