Beki Mtanzania anayeichezea klabu ya Baroka inayoshiriki Ligi
Kuu Afrika Kusini amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwezi Aprili na
Mei 2018 kwa upande wa klabu hiyo.
Mchezaji huyo ameisaidia timu
yake kufunga mabao mawili na kuiwezesha kwenda sare ya mabao 2-2 katika
mchezo wa ligi uliopigwa Aprili 28 dhidi ya Bloem Celtic katika Uwanja
wake wa nyumbani,
Banda amekabidhiwa mpungwa wa rand 5000.00 kama ambavyo klabu hiyo hutoa kiasi cha fedha kwa kila mchezaji bora ndani ya mwezi.
Baroka FC imekshika nafasi ya 12 kwenye msimamo wa Ligi ikiwa imejikusanyia jumla ya pointi 34.
No comments :
Post a Comment