Waziri
wa Sheria wa Israel Mhe. Aleyet Shaked akiagana na Mkurugenzi Mtendaji
wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi mara baada
ya kumaliza ziara yake ya kikazi jana ya kuona ushirikiano uliopo wa
matibabu ya moyo kwa watoto kati ya JKCI na Taasisi ya Okoa Moyo wa
Mtoto (Save a Child’s Heart – SACH) ya nchini Israel. Kulia ni Mganga
Mkuu wa Serikali Prof. Mohammed Kambi.
Waziri wa Sheria wa Israel Mhe. Aleyet Shaked akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) mara baada ya kumaliza ziara ya
kikazi jana katika Taasisi hiyo. Mhe. Shaked alitembelea Taasisi hiyo
jana kwa ajili ya kuona ushirikiano ulipo wa matibabu ya moyo kwa
watoto, kusomesha madaktari na wauguzi kati ya JKCI na Taasisi ya Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart – SACH) ya nchini Israel.
Waziri
wa Sheria wa Israel Mhe. Aleyet Shaked akiangalia makala ya video
inayoonyesha matibabu ya moyo kwa watoto yanayofanywa na madaktari
bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo
Jakaya Kikwete kwa kushirikiana na wenzao wa Taasisi ya Okoa Moyo wa
Mtoto (Save a Child’s Heart – SACH) ya nchini Israel. Tangu mwaka 2015
JKCI kwa kushirikiana na SACH ya nchini Israel wanafanya kambi maalum ya
matibabu ya moyo kwa watoto ambapo watoto wanaokutwa na matatizo
wanatibiwa hapa nchini na wanaokutwa na matatizo yanayohitaji matibabu
ya hali ya juu wanatibiwa nchini humo bila malipo.
Waziri
wa Sheria wa Israel Mhe. Aleyet Shaked akisaini kitabu cha wageni
alipotembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) jana kwa ajili ya
kuona ushirikiano ulipo wa matibabu ya moyo kwa watoto, kusomesha
madaktari na wauguzi kati ya JKCI
na Taasisi ya Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart – SACH) ya nchini
Israel. Kushoto ni Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Mohammed Kambi na
kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
Prof. Mohamed Janabi.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi
akiongea na waandishi wa Habari mara baada ya kumalizika kwa ziara ya Waziri wa Sheria wa Israel Mhe. Aleyet Shaked alipotembelea Taasisi hiyo jana kwa ajili ya kuona ushirikiano ulipo wa matibabu ya moyo kwa watoto, kusomesha madaktari na wauguzi kati ya JKCI na Taasisi ya Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart – SACH) ya nchini Israel.
Picha na JKCI
No comments :
Post a Comment