Saturday, April 28, 2018

MWISHO WA UHAKIKI WA NGOs NCHINI MWEZI MEI, 2018


  Mwakilishi Taasisi ya Twaweza Bi. Anastazia Rugaba akitoa maoni mara baada ya kumalizika kwa mjadala kwenye makundi uliolenga kutoa maoni juu ya uboreshaji wa Sera ya Taifa ya Mashirika Yasiyo ya kiserikali wakati wa  kikao kazi kilichofanyika Jijini Arusha.

NA MWANDISHI WETU- ARUSHA
SERIKALI imeagiza Mashirka yote Yasiyo ya Kiserikali kuhakikisha wanajihakiki katika Ofisi ya Msajili wa Mashirika hayo iliyopo chini ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na ifikapo mwezi Mei mwaka huu na zoezi hilo litasitishwa rasmi.
Hayo yamesemwa leo Jijini Arusha na Msajili wa Mashirka Yasiyo ya kiserikali nchini Bw. Marcel Katemba alipokuwa akifunga kikao kazi cha wadau wa NGOs nchini kilichokuwa kinajadili kuhusu maboresho ya Sera ya Taifa ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali.
Bw. Katemba amesema kuwa zoezi hili limechukua muda mrefu sana na wamekuwa wakiongeza muda mara kwa mara ili kuyapa nafasi mashirika ambayo hayakujihakiki kufanya hivyo.
Ameongeza kuwa mara baada ya kumalizika kwa zoezi hilo mwezi Mei mwaka huu wataweka majina ya Mashirika yote ambayo yatakuwa yamejihakiki kwenye Tovuti mpya ya Msajili na yale yote ambayo yatakuwa hayajajihakiki hayataruhusiwa kufanya kazi nchini.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Mashirika yasiyo ya Kiserikali Bw. Nicholous Zakaria ameishukuru Serikali kupitia Ofisi ya Msajili wa NGOs kwa ushirkiano wanaowapa kama Baraza na kwa wadau wote wa NGOs nchini.

  Mwakilishi Shirika la TAVICO Bw. Charles Nkwabi akitoa maoni mara baada ya kumalizika kwa mjadala kwenye makundi uliolenga kutoa maoni juu ya uboreshaji wa Sera ya Taifa ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali wakati wa  kikao kazi kilichofanyika Jijini Arusha.

  Msajili wa Mshirika Yasiyo ya Kiserikali Bw. Marcel Katemba akitoa neno kwa wadau wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali  mara baada ya kumalizika kwa kikao kazi kilichofanyika Jijini Arusha kilichowakutanisha wadau hao kujadili maboresho ya Sera ya Taifa ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali.

 Mkurugenzi Msaidizi Usajili NGOs Bw. Leornald Baraka akichangia jambo katika mjadala wa wadau wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali uliojikita kujadili maboresho ya Sera ya Taifa ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali wakati wa kuhitimishwa kwa kikao kazi kilichofanyika Jijini Arusha
  Baadhi ya wadau wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali wakiwa katika makundi wakijadili na kutoa maoni kuhusu maboresho ya Sera ya Taifa ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali katika kikao kazi kilichofanyika Jijini Arusha.



Baadhi ya wadau wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali wakiwa katika makundi wakijadili na kutoa maoni kuhusu maboresho ya Sera ya Taifa ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali katika kikao kazi kilichofanyika Jijini Arusha. (PICHA NA KITENGO CHA MAWASILIANO WAMJW)

No comments :

Post a Comment