Saturday, April 28, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mhe. Evod Mmanda apokea vitabu kutoka Taasisi ya Elimu Tanzania (TET)


index1
Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mhe. Evod Mmanda kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara  akipokea vitabu kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), Profesa Benadeta Kiliani .
Vitabu hivyo vya Kiada kwa darasa la 1-4 vinasambazwa na TET kwa kwa mikoa yote Tanzania na leo ilikuwa zamu ya Mtwara.
Hafla fupi ya makabidhiano ya vitabu hivyo imefanyika ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Ufundi Mtwara.
Katika hotuba fupi aliyoitoa Mhe. Mmanda wakati wa mapokezi hayo amesema anaridhishwa na jitihada za serikali ya awam ya tano katika kuinua elimu ya Tanzania.
Kwa upande wake Profesa Benadeta Kiliani amezitaka Halmashauri zote zilizokwisha pokea vitabu hivyo zihakikishe zinavifikisha kwa walengwa ambao ni wanafunzi.
INDEX2

No comments :

Post a Comment