Saturday, April 28, 2018

MAGARI YALIYOBEBA POLISI,WANAJESHI YAPATA AJALI MKOANI MOROGORO


Basi lililokuwa limebeba askari Polisi limegongana na gari dogo aina ya Noah iliyokuwa imebeba Wanajeshi wa JWTZ, katika maeneo ya Bwawani mkoani Morogoro.
IMG-20180427-WA0101
IMG-20180427-WA0104
IMG-20180427-WA0103
Imeelezwa kuwa basi hilo la Polisi lilikuwa likitokea jijini Dodoma kwenye sherehe za Muungano zilizofanyika jana Aprili 26, 2018 huku Noah hiyo iliyokuwa na Wanajeshi takribani 6 pamoja na mtoto ikitokea Morogoro. Majeruhi wote wamepelekwa hospitali Morogoro
IMG-20180427-WA0107
IMG-20180427-WA0102
Hata hivyo, bado hakuna taarifa rasmi lakini habari za awali zinasema askari wawili wamefariki papohapo ingawa  Kamanda wa Polisi, Ulrich Matei amesema atatoa taarifa za kina baaadae.

No comments :

Post a Comment