BENKI KUU YA TANZANIA 
BENKI KUU YA TANZANIA (BoT)
WENYE AMANA BENKI ZINAZOFILISIWA
KUANZA KULIPWA MACHI 28, WADAI, WADAIWA WAPEWA NOTISI
Bodi
ya Bima ya Amana (DIB) imetangaza ya kuwa kuanzia tarehe 28 Machi, 2018 itaanza
kuwalipa fidia ya bima ya amana waliokuwa wateja wa benki tano ambazo
zilitangazwa kufutiwa leseni za kufanya shughuli za kibenki tarehe 4 Januari
mwaka huu.
Aidha,
Bodi hiyo ambayo imepewa mamlaka na Benki Kuu ya Tanzania kuwa mfilisi wa
taasisi hizo, imewataka wadaiwa na wadai wa taasisi hizo kujitokeza kuwasilisha
vithibitisho vya madai yao ifikapo tarehe 17 Aprili, 2018.
Wenye
amana watakaonufaika na malipo hayo ya fidia ya bima ya amana ni waliokuwa
wateja wa Njombe Community Bank Ltd, Meru Community Bank, Covenant Bank for
Women in Tanzania Ltd, Efatha Bank Ltd na Kagera Farmers’ Cooperative Bank Ltd,
ambazo ziko katika ufilisi ambao watatakiwa kutimiza masharti kadhaa ili kupata
malipo yao.
Masharti
yaliyotajwa ni pamoja na kutambua mahali na muda wa malipo, ukomo wa malipo ya
fidia, madai kwa amana zinazozidi shilingi 1,500,000, na kuwa na vitambulisho
stahiki.
NB:
Taarifa zaidi zinapatikana katika mtandao wa Benki Kuu: http:/www.bot.go.tz
No comments :
Post a Comment