Tuesday, March 20, 2018

WAZAZI TUSIGEUZE KITEGA UCHUMI WATOTO WA KIKE/TUWASOMESHE -MSIMBE


1 2
Mwenyekiti wa muungano wa akinamama wa mkoani Pwani ,(Pwani Generation Queens ),Betty Msimbe akizungumza wakati walipotembelea kituo cha kulelea watoto yatima cha Buloma kilichopo kata ya Sofu,Pichandege wilayani Kibaha
3
Mwenyekiti wa muungano wa akinamama wa mkoani Pwani ,(Pwani Generation Queens ),Betty Msimbe (wa kushoto ) akimkabidhi vyakula na vifaa mbalimbali matron wa kituo cha Buloma , Simpho Aidan(wa kulia)
4
Watoto wanaolelewa kituo cha kulelea watoto cha Buloma foundation kilichopo kata ya Sofu ,Pichandege Kibaha wakionyesha vifaa walivyopokea kutoka kwa kikundi cha Pwani Generation Queens ),wakati walipokwenda kuwatembelea na kutoa misaada mbalimbali Sofu.
Picha na Mwamvua Mwinyi
………………
Na Mwamvua Mwinyi,Kibaha
WAZAZI na walezi wameaswa kuacha tabia ya kuwakatisha masomo watoto wao wa kike kwa makusudi ya kuwageuza kitega uchumi kwa kuwaoza kwa vibopa na badala yake wawape haki yao ya elimu .
Aidha jamii imetakiwa kujenga tabia ya kuwawezesha watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu, yatima na vituo vinavyosaidia watoto hao ikiwa ni pamoja na kuwapa mahitaji muhimu hasa elimu, mavazi na malazi.
Rai hiyo ilitolewa na mwenyekiti wa muungano wa akinamama wa mkoani Pwani ,(Pwani Generation Queens ),Betty Msimbe wakati walipotembelea kituo cha kulelea watoto yatima cha Buloma kilichopo kata ya Sofu,Pichandege wilayani Kibaha.
Betty alieleza wakiwa ni wazazi na wanawake wameona watembelee watoto waliopo kituoni hapo na kuwapatia msaada wa mchele kilo 100,mafuta ya kupikia,sabuni za maji ,sabuni za kufulia ,peds ,sabuni za kuoga,unga,sukari,mafuta ya kupika na vifaa mbalimbali .
Alisema vituo hivyo ni msaada mkubwa ambapo husaidia kuishi na watoto waliotelekezwa kwa makusudi,wazazi kutengana ,kutupwa wakiwa wadogo na wengine kukimbia kwa wazazi baada ya kutaka kulazimishwa ndoa za utotoni .
“Sisi kama wazazi tumejitoa kwa kidogo chetu ,naomba wadau wa maendeleo na wenye uwezo wa kifedha ,watembelee vituo na kutoa misaada kwa watoto hawa kwa kushirikiana na serikali pia” alisema Betty.
Hata hivyo ,alisikitishwa kuona kuna msichana ambae alifikishwa kituoni hapo kupitia ustawi wa jamii kutokana na mzazi wake wa kiume kutaka kumkatisha masomo ili amuoze.
“Wazazi tuache tamaa ,yaani unamuachisha mtoto wako shule kisa umfanye mtaji ,upate fedha ,tuwasomeshe watoto wetu wa kike kwani nao ni sawa na wale wa kiume”
“Tusiwabague watoto kwa jinsia zao ,kila mmmoja ana haki ya kupata elimu ‘” alisisitiza Betty.
Akizungumzia kuhusu muungano huo ,alifafanua kuwa wapo kikatiba wana wanachama 75 ,wana akaunti na fedha ya akiba sh. mil .Tisa ,wanaendelea na miradi midogo ambapo wanatarajia kusheherekea mwaka mmoja wa umoja wao ifikapo april 8 mwaka huu.
Makamu Mwenyekiti wa Pwani generation queens , Elizabeth Ngai ,alisema kutoa ni moyo na sio utajiri,hivyo jamii iwatupie jicho watoto yatima ili wafikie ndoto zao.
Alisema watoto hao wengi wao wamefikia hapo kutokana na matatizo ya wazazi na walezi wao na hawakukusudia kuishi maisha waliyonayo.
Nae mtoto anaelelewa katika kituo hicho Neema Madei ,alisema baba yake alimkatisha masomo akiwa na miaka 12 ili amuozeshe kwa mtu kama babu yake .
Alielezea ,mama yake alikuwa nae pamoja ambapo alifikisha taarifa hiyo ustawi wa jamii ambao walimpeleka kituo cha Buloma foundation na sasa yupo darasa la tano .
“Nawashukuru ustawi wa jamii kwa kufungua maisha yangu kwakuwa sikutaka kuolewa ,na nawaasa wazazi wenye tamaa waache tamaa zao na wawasomeshe watoto wao wakike ,wasikimbilie fedha waangalie haki za watoto” alisisitiza Neema.
Kwa upande wake ,matron wa kituo cha Buloma , Simpho Aidan ,alisema wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa uzio ,bima ya afya kwa ajili ya watoto hao na jengo la watoto wakiume.
Aliwaomba wadau wenye uwezo wawaunge mkono ili kuondoa changamoto hizo.
Simpho alisema ,kituo hicho kinawalea watoto 38 ,na wapo ambao wamefika kidato cha tano na sita na wengine wanasoma chuo cha ufundi (VETA).

No comments :

Post a Comment