Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Aggrey
Mwanry akisisitiza umuhimu wa wananchi kulinda miundombinu ya barabara
katika kijiji cha Imalamakoye katika jimbo la Urambo wakati wajumbe wa
Kamati ya Bunge ya Miundombinu walipokagua ujenzi wa barabara Tabora-
Urambo-Kaliua inayojengwa kwa kiwango cha lami, kulia ni Naibu Waziri wa
Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano (sekta ya ujenzi) Mhe. Elias John
Kwandikwa.
Muonekano wa barabara ya kutua na kurukia ndege ambayo ujenzi wake umekamilika katika uwanja wa ndege wa Tabora.
Muonekano wa barabara ya
Mwigumbi-Maswa KM 50.3 ambayo ujenzi wake kwa kiwango cha lami
umekamilika barabara hiyo ni sehemu ya barabara ya
Mwigumbi-Maswa-Bariadi-Lamadi KM 171.8
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya
Miundombinu Mhe. Moshi Selemani Kakoso akifafanua jambo kwa Naibu
Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano (sekta ya ujenzi) Mhe. Elias
John Kwandikwa wakati Kamati hiyo ilipokagua ujenzi wa barabara ya
Mwigumbi-Maswa-Bariadi-Lamadi KM 171.8 inayojengwa kwa kiwango cha lami,
wengine ni wajumbe wa kamati hiyo wakifuatilia.
Naibu Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na
Mawasiliano (sekta ya ujenzi) Mhe. Elias John Kwandikwa akifafanua
jambo kwa wajumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Miundombinu
walipokagua ujenzi wa barabara ya Mwigumbi-Maswa-Bariadi-Lamadi KM 171.8
inayojengwa kwa kiwango cha lami.
……………….
Naibu Waziri wa Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano anaeshughulikia (sekta ya ujenzi), Mhe. Elias
John Kwandikwa amesema Serikali inaendelea kuwalipa wakandarasi wa
barabara madeni yao ya zamani nay a sasa ili kuwawezesha kuongeza kasi
katika miradi mipya ya ujenzi wanayopewa.
Mhe. Kwandikwa ameiambia Kamati ya
Bunge ya Miundombinu kuwa tayari kiasi cha shilingi bilioni 400
kimelipwa kwa wakandarasi katika muda mfupi ikiwa ni mkakati
wakuwawezesha kuwa na kasi katika miradi mingine ya ujenzi inayoendelea.
“Tumejipanga kuhakikisha madeni ya
ujenzi wa barabara yanalipwa kwa wakati ili tuwe na nguvu ya kuwabana
wakandarasi kumaliza miradi kwa wakati”, amesisitiza Naibu Waziri
Kwandikwa.
Amesema nia ya Serikali ni
kuziwezesha barabara kuu na za mikoa kufunguka kwa lami ili kupunguza
mzunguko kwa njia nyingi na kuiunganisha mikoa na wilaya kiurahisi na
hivyo
kuchochea shughuli za kilimo,mifugo,uvuvi na biashara nchini kote.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya
Miundombinu Mhe. Moshi Sulemani Kakoso amesisitiza umuhimu wa barabara
zinazojengwa kuwekewa maeneo maalum ya kuvusha mifugo ili zidumu kwa
muda mrefu na kusisitiza umuhimu wa kuwawezesha wakandarasi wa ndani
katika miradi midogo ili kuwajengea uwezo.
“Hakikisheni mnakuwa na programu
endelevu za kuwawezesha wakandarasi wa ndani ili baadhi ya miradi
waitekeleze wenyewe na hivyo kukuza uwezo wa kitaalamu na kiuchumi”,
amesema Mhe. Kakoso.
Aidha Mwenyekiti huyo wa kamati ya
miundombinu amesisitiza umuhimu wa kuwaelimisha wananchi umuhimu wa
barabara za lami ili badala ya kuzihujumu kwa kuharibu miundombinu yake
wazilinde na kuzitumia kuibua fursa za kiuchumi na kijamii katika maeneo
yao.
Kamati ya Bunge ya Miundombinu iko
katika ziara ya kutembelea miundombinu inayosimamiwa na Wizara ya
Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano katika mikoa ya Shinyanga, Simiyu,
Mwanza, na Mara.
Imetolewa na Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano
No comments :
Post a Comment