Wednesday, March 21, 2018

PROF. KABUDI ATEMBELEA UJENZI WA MAHAKAMA KUU MKOANI MARA


IMG-20180320-WA0017
Mhe. Waziri  wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi akisign kitabu cha wageni alipofika eneo ambalo ujenzi wa Mahakama Kuu unafanyika
IMG_20180320_140708
Waziri mhe. Prof. Palamagamba Kabudi akisikiliza maelezo ya awali kuhusiana na mradi wa ujenzi Mahakama Kuu mkoani Mara unaoendelea mjini Musoma
IMG_20180320_142419
Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi akizungumza kitu baada ya kutembelea na kujionea maendeleo ya ujenzi wa Mahakama hiyo mjini Musoma
IMG_20180320_142733
Prof. Kabudi  na timu aliyoambatana nayo akizungumza  na mkuu wa Wilaya ya Bunda kuhusiana na Mahakama ya wilaya hiyo
IMG_20180320_142848
Prof. Kabudi akizungumza na kinana wa kitanzania ambaye ni mtaalamu wa quantity surveyor ambaye anajumuisha timu ya wataalamu wanaojihusishs na ujenzi wa jengo hilo
……………………
Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba ametembelea mradi wa  ujenzi wa Mahakama Kuu mkoani Mara na kujionea ujenzi huo unavyoendelea mjini Musoma
Akizungumza baada ya kupata taarifa fupi kuhusu ujenzi wa Mahakama hiyo na kuutembelea
Prof. Kabudi amewataka wasimamizi wa mradi huo kuutangaza kwani uwepo wa Mahakama Kuu mkoani Mara kutaleta ahueni kubwa kwa wananchi wa mkoa huo ambao walikuwa wanalazimika kwenda Mwanza kutafuta haki zao.
Mhe. Waziri amesema  Mahakama hiyo itakapokamilika wananchi wa mkoa wa Mara watapata haki zao kwa wakati ndani ya mkoa wao bila ya kulazimika kwenda umbali mrefu kutafuta haki.
Ujenzi wa Mahakama Kuu mkoani Mara unatekelezwa kupitia  mpango mkakati wa miaka mitano wa Mahakama wa 2015/2020 ambao unatoa kipaumbele kwa ujenzi wa miundombinu ya Mahakama nchini ili kusogeza huduma za Mahakama karibu na wananchi

No comments :

Post a Comment