Ni Mbunge wa Jimbo la Hanang,Mkoani
Manyara,DK.Mary Nagu (wa kwanza kutoka kushoto) akimpongeza aliyekuwa
diwani wa Kata ya Gihandu,Mathayo Semuhenda mara baada ya kutangaza
azma yake ya kujiunga na CCM.
Ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa
Manyara,Simon Lulu akipokea kadi ya Chama Cha ACT Wazalebdo kutoka
kwa aliyekuwa diwani wa kata ya Gihandu,Mathayo Semuhenda.
Ni Aliyekuwa diwani wa kata ya
Gihandu kwa tiketi ya ACT Wazalendo, MATHAYO SEMUHENDA akipokea kadi
ya CCM baada ya kutangaza azma yake ya kujiunga na CCM.
Ni Aliyekuwa diwani wa kata ya
Gihandu,Mathayo Semuhenda akila kiapo cha uadilifu mara baada ya
kukabidhiwa kadi ya chama cha mapinduzi(CCM).
Na Jumbe Ismaily
ALIYEKUWA diwani wa kata ya
Gihandu,wilayani Hanang,Mkoani Manyara kwa tiketi ya Chama cha ACT
Wazalendo,Mathayo Samuhenda amejiuzulu udiwani wa kata hiyo na
kujiunga na Chama Chama Mapinduzi (CCM).
Akitangaza azma yake hiyo ya
kujiuzulu katika nafasi yake ya udiwani wa kata hiyo kwenye mkutano
wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya shule ya msingi
Gihandu,Samuhenda alisisitiza kwamba aliamua kujiuzulu na kuwaacha
wapiga kura wake siyo kwa njia ya ukatili bali alifikia maamuzi hayo
kwa lengo la kuwaunganisha wananchi wote wa kata hiyo.
No comments :
Post a Comment