Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akiteta na Kamishina Jenerali wa mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na
Dawa za Kulevya, Rogers Siyanga wakati alipozindua kliniki ya Methadone
kwa ajili ya waathirika wa dawa za kulevya kwenye hospitali ya Sekou
Toure jijini Mwanza Februari 20, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Baadhi ya waathirika wa dawa za
kulevya wanaohudumia na Kliniki ya Methadone iliyopo katika hospitali
ya Sekou Toure jijini Mwanza, wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
wakati alipozungumza baada ya kuzindua kliniki hiyo, Februari 20, 2018.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akikata utepe kuzindua Muongozo wa Uendeshaji wa Nyumba za Waathirika wa
Dawa za Kulevya (Sober House) kwenye hospitali ya Sekou Toure jijini
Mwanza, Februari 20, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
…………………………………………………………………..
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka Watanzania wakiwemo wakazi wa mkoa wa Mwanza kuachana na biashara ya dawa za kulevya.
Pia Waziri Mkuu amegiza vijana
nchini waelimishwe madhara mbalimbali yanayosababishwa na matumizi ya
dawa za kulevya ili wajiepushe nazo.
Waziri Mkuu aliyasema hayo jana
(Jumanne, Februari 20, 2018) alipozindua kliniki ya methadone kwa ajili
ya waathirika wa dawa za kulevya.
Alizindua kliniki hiyo iliyopo
kwenye hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Mwanza ya Sekou Toure akiwa katika
siku ya sita ya ziara yake ya kikazi mkoani Mwanza.
“Serikali imejizatiti katika vita
dhidi ya biashara ya dawa za kulevya, hivyo nawataka wananchi
wasijishughulishe nayo. waache kutumia, kusambaza na kuuza.”
Pia aliwaomba wananchi
washirikiane na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya kwa
kutoa taarifa za watu wanaojihusisha na dawa hizo.
Kwa upande wake, Kamishna
Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Bw.
Rogers Siyanga aliishukuru Serikali kwa kutambua madhara ya dawa za
kulevya na kuchukua hatua.
Bw. Siyanga alitumia fursa hiyo
kutoa wito kwa waathirika wa dawa za kulevya kwenda katika kliniki za
methadone ili wapatiwe matibabu yatakayowafanya kuachana na matumizi ya
dawa hizo.
Naye, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Bw.
John Mongella alisema kuwa, mkoa huo ni miongoni mwa waathirika wakubwa
wa biashara ya dawa za kulevya. Aidha, aliongeza kuwa bado kuna watu
wanaoendeea kujishughulisha na biashara hiyo na kwamba Mkoa unaendelea
kupambana nao.
Kwa upande wake, Naibu Waziri wa
Afya na Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine
Ndungulile alisema dawa za kulevya zinasababisha madhara makubwa katika
sekta ya afya kwa kuwa yanachangia kusambaa kwa magonjwa mbalimbali
yakiwemo ukimwi na kifua kikuu.
Pia alisema kwa sasa dawa za
methadone zinazotolewa kwa waathirika wa dawa za kulevya wanazipata
kutoka kwa wahisani mbalimbali. Hata hivyo, Serikali imepanga kuingiza
suala hilo katika bajeti ijayo ili ianze kuagiza y
No comments :
Post a Comment