Monday, February 26, 2018

DC SALAMA AWAOMBA WAZAZI NA WALEZI SHEHIA YA MAKANGALE KUKUBALIANA NA MAAMUZI ATAKAYOCHUKUA DHIDI YA VIJANA WANAOJIHUSISHA NA VITENDO VYA UHARIFU VISIWANI PEMBA

DSC_0827
Na Masanja Mabula – Pemba
MKUU wa Wilaya ya Micheweni Salama Mbarouk Khatib amewaomba wazazi na walezi katika Shehia ya Makangale kukubaliana na maamuzi atakayochukua dhidi ya vijana wanaojihusisha na vitendo vya uhalifu katika shehia hiyo.
Amesema kila mzazi anapaswa kuyaunga mkono maamuzi hayo kwani lengo ni kurejesha maadili kwa vijana ambayo yanazidi kuporomoka kutokana na waliowengi kujiunga na vikundi vya ulevi.

Akizungumza na wananchi wa shehia hiyo , kwenye kikao cha kusikiliza kero za jamii , Salama amewaonya wazazi ambao wataingilia maamuzi yake na kusema atawajumuisha kwenye orodha ya wahalifu.
‘Ninayo orodha ya vijana wanajihusisha na vitendo vya ulevi , naomba sana wazazi msingilie maamuzi yangu , na atakaye ingilia nitakuwa sahaani moja naye ’’alisisitiza.
Aidha Mkuu huyo wa Wilaya ameelezea kusikitishwa na baadhi ya wananchi wa shehia hiyo kufungua klabu za kuanza kuuza pombe bila ya kuwa na kibali na kuutaka uongozi wa shehia kuzifunga .
Mapema mwakilishi wa wananchi haaaaao Rashid Habib amesema maadili kwa vijana yanazidi kuporomoka , kwani baadhi ya vijana wanajiingiza katika vitendo vya unywaji wa pombe .
Amesema hali hiyo imesababishwa na ongezeko la klabu za pombe mabazo zimefikia nne , na hivyo kuwafanya vijana kujiingiza kwenye vikundi viovu .
‘Hili pia limesababisha ongezeko la vitendo vya wizi wa mazao pamoja na mifugo , hivyo tunaomba nguvu kutoka serikalini tumechoka kwani tumeanza kunyemelewa na umaskini’’ alisema.
Naye Rehema Makame amesema  uwepo wa vijana wanaojihusisha na ulevi unawanya wavunjike moyo kuendelea na shughuli za kilimo cha zao la mwani .
Amesema baadhi ya vijana wanashindwa kuwakemea kwa hofu ya kupokea kipigo kwani huwa wamevuta bangi na wakati mwengine kunywa pombe hivyo chochote wanaweza kukifaanya .

No comments :

Post a Comment