Naibu Waziri wa Maliasili na
Utalii, Japhet Hasunga (kushoto) pamoja na Katibu Mkuu wa Maliasili na
Utalii, Maj. Gen. Gaudence Milanzi (kulia) wakizungumza na Mbunge wa
viti maalumu, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya
Ardhi, Maliasili na Utalii, Zainabu Mwamwindi wakiwa wameongozana na
Wajumbe Kamati hiyo wakati walipotembelea jana Jengo la Makumbusho ya
Olduvai ya Gorge ambako ni chimbuko la historia ya Binadamu katika
Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro.
Katibu Mkuu wa Maliasili na
Utalii, Maj. Gen. Gaudence Milanzi (kulia) akizungumza na Naibu Waziri
wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kushoto) wakiwa na Wajumbe
Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Ardhi, Maliasili na Utalii wakati
walipotembelea jana Jengo la makumbusho ya Olduvai ya Gorge ambako ni
chimbuko la historia ya Binadamu katika Mamlaka ya Hifadhi ya
Ngorongoro
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya
Kudumu ya Ardhi, Maliasili na Utalii , Kemilembe Luota ( wa kwanza
kushoto) Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga
(katikati) pamoja na Katibu Mkuu wa Maliasili na Utalii Maj. Gen.
Gaudence Milanzi (wa pili kulia) wakiwa na baadhi ya Wajumbe wa kamati
hiyo wakiwa kwenye ‘’View Point’ kituo ambacho hutumika kuangalia
bonde la Ngorongoro kabla ya kutelemka katika Bonde hilo jana wakati
walipofanya ziara ya kutembelea Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro
Huyu ndiye Faru Fausta ni faru
kikongwe kuliko wote nchini, akiwa na umri wa miaka 54, na anahitaji
matunzo mazuri ili aendelee kuvuta watalii na wanasayansi kutoka kila
pembe ya dunia.
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya
Bunge ya Kudumu ya Ardhi, Maliasili na Utalii na Waandishi wa habari
wakiji’selfie’ katika banda la Faru Fausta ambaye ndiye faru kikongwe
kuliko wote nchini, akiwa na umri wa miaka 54, na anahitaji matunzo
mazuri ili aendelee kuvuta watalii na wanasayansi kutoka kila pembe ya
dunia wakati walipotembelea banda hilo kwa ajili ya kujionea
Baadhi ya Msururu wa Magari
yaliyokuwa yamewbeba wjumbe wa kamati ya Bunge ya Kudumu ya Ardhi,
Maliasili na Utalii pamoja na viongozi na watumishi wa Wizara pamoja na
wa Ngorongoro kwa ajili ya kutelemka kwenyeBonde la Ngorongoro.
Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya
Bunge ya Kudumu ya Ardhi, Maliasili na Utalii wakiwa katika nje ya
ofisi ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kwa ajili ya kuanza ziara.
Kundi la Simba wakiwa wamepumzika
walipoonekana jana wakati Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Ardhi, Maliasili
na Utalii ilipofanya ziara ya kutembelea Bonde la Ngorongoro.
Bonde la Olduvai Gorge ambako ni
chimbuko la historia ya binadamu ni kivutio cha kinachowavuta watalii
wengi kutembelea eneo hilo.
Naibu Waziri wa Maliasili na
Utalii, Japhet Hasunga( wa kwanza kushoto) akiteta jambo na
Wakurugenzi wa Wizara hiyo wakati wa ziara ya Kamati ya Bunge ya Kudumu
ya Ardhi, Maliasili na Utalii ilipotembelea jana Makumbusho ya Olduvai
Gorge
(PICHA ZOTE NA LUSUNGU HELELA –MALIASILI NA UTALII
…………………
Kamati ya Bunge ya Kudumu ya
Ardhi, Maliasili na Utalii imeipongeza Mamlaka ya Hifadhi ya
Ngorongoro kwa kazi nzuri iliyofanya ya ujenzi wa jengo la makumbusho
ya kisasa katika Bonde la Olduvai ya Gorge ambako ni chimbuko la
historia ya Binadamu.
Kamati hiyo imesema imeridhishwa
na ujenzi wa jengo hilo ambalo litawavutia watalii na wanasayansi
wabobezi wa masuala ya Malikale kutembelea Makumbusho hiyo.
Kamati hiyo ilibainisha kuwa
Makumbusho hiyo mbali ya kutumika kuingiza pesa kupitia watalii pia
inatumika kama kielelezo na utambulisho muhimu wa taifa katika
kutangaza utamaduni wa Mtanzania ndani na nje ya nchi.
Hayo yalisemwa jana na Kamati hiyo
wakati ilipofanya ziara ya kutembelea Ngorongoro Crater na
Makumbusho ya Olduvai Gorge katika Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo.
Kemilembe Luota ameipongeza Serikali pamoja na wataalamu kwa kazi nzuri
waliyoifanya kwa kuhakikisha kuwa eneo la Olduvai Gorge linakuwa
kivutio bora kwa ajili ya historia ya nchi na kivutio kikubwa cha Utalii
duniani.
‘’ Sisi kama Kamati tunaipongeza
Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kwa kuyafanyia kazi mapendekezo yote
tuliyoyatoa kwa mara ya kwanza tulipokuja kwa vile tumeona kazi nzuri
imefanyika.’’
Katika hatua nyingine, Mwenyekiti
huyo ametoa wito kwa wananchi kutembelea makumbusho hiyo kwa vile idadi
ya watalii wa ndani aliyokutana nayo sio ya kuridhisha.
Naibu Waziri wa Maliasili na
Utalii, Japhet Hasunga amesema makumbusho hiyo inatoa ushahidi dhahiri
kuwa hata wazungu, mababu zao walitoka Afrika.
Mjumbe wa Kamati hiyo ambaye pia
ni Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye amesema Makumbusho hiyo hadi hapo
ilipofikia imeboreshwa kwa kiwango cha hali ya juu hata hivyo ameitaka
Wizara ihakikishe inaitangaza ipasavyo ili watalii wengi zaidi wazidi
kutembelea.
Awali, Mhifadhi Mkuu wa Mamlaka
hiyo, FredyManongi amesema tangu kuzinduliwa kwa makumbusho hiyo kwa
wiki moja imekuwa ikipokea zaidi ya watalii wapatao 40000 hali
inayopekelea kuwa ni miongoni mwa Makumbusho inayofanya vizuri zaidi
barani Afrika
No comments :
Post a Comment