Friday, December 22, 2017

WATANZANIA WATAKIWA KUICHUKULIA LUGHA YA KISWAHILI KAMA FURSA


IMG-20171222-WA0000
Na Florah Raphael.
Kampuni ya Viva Legency inayohusika na mafunzo na ushauri elekezi imekuja na kitabu kinachojulikana kama “Sote Tunaweza” kikiwa na lengo la kusaidia harakati za mabadiliko pamoja na kukuza utamaduni wa mtanzania.
Akiongea na waandishi wa habari Leo jijini Dar es salaam, Mtendaji mkuu wa Vivalegency Fortunata Meela Temu amesema kuwa kitabu cha “Sote Tunaweza” kimeandikwa kwa lugha ya kiswahili na kinampa msomaji uwezo mkubwa wa kubadili fikra na kupiga hatua ya kimaendeleo.

“Kitabu cha sote tunaweza kimeandikwa kwa lugha ya kiswahili na kinampa uwezo msomaji kubadili kifikra na kupiga hatua kiamaendeleo” amesema Fortunata
Pia amesema kuwa katika uandishi wa kitabu hicho wanetumia mifano ya watu mbalimbali kutoka Tanzania na sehemu nyingine za dunia waliofanikiwa na kusema kuwa wametumia mifano hiyo ili kumtia hamasa msomaji na kumfanya kufuata nyendo za hao watu waliofanikiwa.
“Kitabu hiki tumetumia mifano ya watu waliofanikiwa kutoka Tanzania na sehemu nyingine ili kumpa msomaji hamasa ya kufuata nyendo zao” amesema Fortunata.
Pia Fortunata ameongeza kuwa mafanikio yanaweza kupatikana kwa kuangalia fursa zinazopatikana ndani ya jamii hivyo kuwataka watanzania kutumia lugha ya kiswahili kama fursa kwa kuhabarishana na kuelimishana .
Kwa upande wake Naibu katibu mkuu Wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi Dr.AveMaria Semakafu ameipongeza kampuni ya Vivalegency na kusema kuwa kitabu cha “sote tunaweza” kimekuja wakati mwafaka kwa sababu nchi yetu ipo kwenye harakati za mabadiliko kuelekea uchumi wa kati.
“Sote tunaweza kimekuja wakati mwafaka kwa sababu nchi yetu IPO kwenye harakati za mabadiliko kuelekea uchumi wa kati” amesema Dr.Semakafu.
Pia amebainisha kuwa Tanzania inachangamoto kubwa katika utamaduni wa uandishi na usomaji vitabu na kuwaomba watanzania watumie fursa ya kuandika vitabu vyenye dhima yenye kuleta maana na kuachana na utamaduni wa kuandika vitabu ambavyo havina dhima yoyote ya kubadili fikra na kuleta chachu ya maendeleo.

No comments :

Post a Comment