Tuesday, December 12, 2017

TBL YANG’ARA TUZO YA MWAJIRI BORA 2017 ‘KINARA KWA KUVUTIA NA KUENDELEZA VIPAJI VYA WAFANYAKAZI WAKE’

TBL TUZO 1
Naibu Waziri ,Ofisi ya Waziri Mkuu(Watu wenye ulemavu ) Stella Ikupa,akimkabidhi  mkurugenzi wa raslimali watu wa TBL Group, David Magese, tuzo ya ushindi wa jumla katika kipengele cha kuajiri na kukuza vipaji vya wafanyakazi kutoka Chama cha Waajiri Tanzania (ATE)  hafla ya tuzo hizo ilifanyika katika ukumbi wa Mlimani City  jijini Dar  es Salaam.(Kulia) ni Mkurugenzi Mkuu wa Chama cha Waajiri Tanzania,Dk.Aggrey Mlimuka
5/8.Baadhi ya wafanyakazi wa TBL Group wakishangilia mafanikio ya kampuni yao katika ukumbi wa Mlimani City baada ya kampuni yao kuibuka kidedea
 
………………….
Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) imepata tuzo kutoka Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE) ya utekelezaji vigezo vya Raslimali Watu kwa viwango vinavyotakiwa na kuwa kinara katika kipengele cha kuwa na mazingira bora ya ajira , kuajiri wafanyakazi wenye vipaji na kuendeleza vipaji vyao .Mbali na tuzo hii kwa kipindi cha miaka 2 mfululizo iliyopita iliibuka mshindi wa jumla wa tuzo ya mwajiri bora nchini.
Hafla ya Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) ya kutoa  tuzo kwa makampuni kwa mbalimbali yanayokidhi viwango bora vya  Raslimali Watu katika vipengele mbalimbali vilivyowekwa na chama hicho ilifanyika katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam ambapo mgeni Rasmi alikuwa ni Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera,Kazi na Ajira,Vijana na Walemavu,Mh.Jenesta Mhagama, aliyewakilishwa na Naibu Waziri wake ,Mh. Stella Ikupa,  ambapo kampuni ya Coca-Cola iliibuka mshindi wa tuzo ya Mwajiri bora na kampuni ya Geita Gold Mine mshindi wa pili.
 TBL TUZO 5
Akiongelea ushindi wa tuzo hii,Mkurugenzi Raslimali Watu wa TBL Group,David Magese,alisema kuwa ushindi huu ni heshima kubwa kwa kampuni kwa kuona mchango inaoutoa kupitia uwekezaji wake unatambuliwa “Tuzo za aina hii tunazoendelea kuzipata zinazidi kututia moyo na tuzo hii sio ya kampuni bali ni ya wafanyakazi wote ,tunajivunia kuona kampuni yetu inaongoza kwa kuwa na mazingira bora yanayovutia kufanyia  kazi na tutaendelea kuyaboresha zaidi siku hadi siku”
Aliongeza kusema kuwa kampuni inaendelea na mkakati wa kutoa mafunzo ya ndani na nje kwa wafanyakazi wake kukuza ujuzi na vipaji vyao sambamba na mafunzo ya ziada ambayo yanawasaidia katika maisha yao ya kila siku nje ya sehemu ya kazi,  kama mafunzo yaliyoendeshwa kwa wafanyakazi wa kampuni ya jinsi ya kutumia fedha zao kwa ufanisi badala ya kuzitumia bila mpangilio na mambo yasiyo ya lazima.
Mbali na mafunzo hayo alisema kuwa kampuni imekuwa na mpango wa kuwapatia ujuzi wafanyakazi wake wanawake kupitia jukwaa lao la TBL Women’s Forum,ambapo wananufaika kwa kupatiwa mafunzo ya mbinu za ujasiriamali na kujadili jinsi ya kukabiliana na changamto mbalimbali zinazosababisha wanawake kubaki nyuma.

No comments :

Post a Comment