Rais wa
Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli hii leo
akihutubia katika sherehe za miaka 56 ya Uhuru wa Tanzania Bara
ametangaza kuwasamehe wafungwa 61 waliokuwa wamehukumiwa kunyongwa.
Akihutubia
mamia ya Watanzania na wageni mbalimbali waliokuwa wamefurika katika
uwanja wa Jamuhuri mjini Dodoma, Rais Dkt. Magufuli pia ametangaza
msamaha kwa familia ya Nguza Viking maarufu kwa jina la Babu Seya pamoja
na mtoto wake Papii Kocha waliokuwa wamehukumiwa kifungo cha maisha
gerezani.
No comments :
Post a Comment