Mhandisi wa Maji Mkoa wa Singida
Lydia Joseph (aliyevaa kofia nyeupe) akiendelea na ukaguzi wa bwawa la
Rungwa-Itigi, nyuma yake ni Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Serikali za
Mitaa Mwajabu Nyamkomola.
Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya
Serikali za Mitaa Mwajabu Nyamkomola akiwa na watendaji wa serikali na
wawakilishi wa Mkandarasi wa bwawa la Rungwa wakitembelea eneo la Bwawa
hilo mapema jana.
Baadhi ya vibarua wakiendelea na
zoezi la kuchanganya zege kwa ajili ya ujenzi wa ukuta katika bwawa la
Rungwa – Itigi, Serikali Mkoani Singida imeagiza kazi hio ifanywe na
mashine ili kuleta ufanisi na kasi huku vibarua hao wakitakiwa kuendelea
na kazi nyingine katika bwawa hilo.
Sehemu ya Bwawa la Rungwa –Itigi
linalojengwa na serikali kwa zaidi ya shilingi milioni mia saba ili
kutatua kero kubwa ya maji katika kijiji cha Rungwa.
……………..
Mkandarasi
anayejenga bwawa la Rungwa katika Halmashauri ya Itigi amepewa siku
saba na Serikali Mkoani Singida kuhakikisha anapeleka vifaa muhimu
vitakavyoongeza kasi na ufanisi wa ujenzi wa bwawa hilo.
No comments :
Post a Comment