Saturday, December 23, 2017

MAJALIWA AZIAGIZA HALMASHAURI ZA WILAYA NCHINI KUSIMAMIA KILIMO CHA ZAO LA PAMBA ILI LIWE NA TIJA

1
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza katika kikao na wadau wa pamba kilichofanyika mjini Shinyanga. Wengine picha ni kuanzia kushoto ni Waziri Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage na Waziri wa Kilimo, Dk. Charles Tizeba.
2
Sehemu ya wakuu wa mikoa inayolima zao pamba wakifuatilia matukio katika kikao cha wadau wa pamba kilichofanyika mjini Shinyanga
3
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa (katikati mwenye miwani) akifurahia wimbo na viongozi wengine mara baada ya kuwasili ukumbini kwa ajili ya kikao hicho. Wengine pichani kuanzia kushoto ni Waziri Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage, Waziri wa Kilimo, Dk. Charles Tizeba na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack.
4
Wakuu wa wilaya za Shinyanga ambazo ndizo miongoni mwa wakulima wa pamba, kuanzia kushoto ni Fadhil Nkurlu (Kahama), Nyabaganga Taraba (Kishapu) na Josephine Matiro (Shinyanga) na kulia pichani Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk. Rehema Nchimbi wakifuatilia matukio.
5
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu ikiwa ni miongoni mwa wakulima wakubwa wa pamba, Stephen Magoiga (mwenye kaunda suti aliyeshika karatasi) akifuatilia matukio katika kikao hicho.
6
Sehemu ya wakuu wa mikoa wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati akizungumza kwenye kikao cha wadau wa pamba kilichofanyika mjini Shinyanga.
7
Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete akichangia katika kikao hicho cha wadau wa pamba.
8
Mbunge wa Kishapu, Suleiman Nchambi akichangia katika kikao.
9
Waziri wa Kilimo, Dk. Charles Tizeba akizungumza wakati wa kikao hicho.
10
Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanry akitoa neno katika kikao hicho.
………………
Na Robert Hokororo, Ofisi ya Mkurugenzi Kishapu
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameziagiza halmashauri za wilaya nchini kuhakikisha zinasimamia kikamilifu kilimo cha zao la pamba ili kiwe na tija.
Ametoa agizo hilo katika kikao na wadau wa pamba kilichofanyika mjini Shinyanga ambapo alizitaka halmashauri hizo kuratibu shughuli za kilimo hicho kwa kuwapangia ratiba maafisa ugani kuwatembelea wakulima kuwapa elimu.

Akizungumza katika kikao hicho kilichoikutanisha mikoa zaidi ya 10 inayolima pamba aliwataka watendaji wakuu wa halmashauri hizo kuhakikisha kila kata na kijiji kunawepo na maafisa ugani ili wasimamie kikamilifu kilimo.
Majaliwa aliwataka maafisa ugani waliopo katika halmashauri hizo kuwafikia wakulima mashambani ili kuwapa elimu na kutatua changamoto zinazowakabili kuhusu kilimo hususan cha pamba.
“Tunataka kuhahakikisha pamba inaleta heshima na inaongeza mapato ya mkulima mmoja mmoja na hata taasisi zetu yaani halmashauri na mikoa zinaingiza mapato kupitia zao la pamba hivyo kila mmoja awajibike,” alisisitiza.
Pia, aliagiza pia ziweke mpango kazi wa namna ya kukiletea mafanikio kilimo hicho huku akisisi kuwa na kwamba atafanya ziara kukagua akisema atataka apewe taarifa ya maendeleo ya kilimo hicho.
Aidha alizitaka halmashauri kuwa na takwimu za misimu ya pamba na ziwe zimehifadhiwa vizuri kwenye kompyuta ili popote zikihitajika zipatikane kwa urahisi.
“Tumejipanga kusimamia zao la pamba kwani awali uzalishaji haukuwa mzuri mkulima anatumia nguvu nyingi sasa tutasimamia kikamilifu kuanzia maandalizi hadi masoko,” alisema Majaliwa.
Katika hatua nyingine aliwataka wadau wa kilimo cha pamba maarufu kama dhahabu nyeupe watimize wajibu ili kukifanya kiwe na tija hivyo kuinua uchumi.
Majaliwa pia aliagiza wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA) kujipanga na kuelekeza kuhusu dawa zilizo bora kwa ajili ya zao hilo na Bodi ya Pamba iwajibike kufuatilia maendeleo yake.
Mkutano huo umewakutanisha pia mawaziri wenye dhamana ya Kilimo, Dk. Charles Tizeba, Viwanda na Uwekezaji, Charles Mwijage, wakuu wa mikoa, wilaya, makatibu tawala, wabunge, wakurugenzi wa halmashauri, taasisi za kilimo, wakulima na wanunuzi wapamba.
PICHA ZOTE NA ROBERT HOKORORO

No comments :

Post a Comment