Thursday, November 9, 2017

Mifuko ya hifadhi ya jamii na huduma ya mikopo ya elimu nchini

A graduation ceremony in Kenya: Not many people are going for science-based disciplines. PHOTO | FILE

Baadhi ya wanafunzi waliofuzu masomo yao wakiwa katika kusherekea mahafari yao. Mfuko wa mafao ya kustaafu wa GEPF ukiwa mojawapo ya mifuko ya hifadhi ya jamii nchini kwa sasa unatoa mkopo wa elimu"Kamata Madigrii na GEPF" kwa mwanachama yeyote aliyesajiriwa na mfuko huu, ili kusaidia kukuza maendeleo ya kijamii na ya kiuchumi nchini.

Na Christian Gaya
Elimu ni nyezo muhimu katika maisha ya binadamu. Kutokana na nguvu ya elimu katika kukuza uchumi wa nchi, mataifa mengi duniani yaliyopata maendeleo ya kijamii na kiuchumi yamewekeza katika sekta ya elimu. Hakuna taifa lolote duniani ambalo linaweza kupata maendeleo bila watu wake kuwa na ...
elimu na kwa maana hiyo hakuna maendeleo bila elimu.
Elimu ndiyo inamfanya binadamu kuwa daktari, rubani, mhandisi na mtaalamu katika nyanja mbalimbali. Kwa kutambua hilo uwekezaji katika sekta hiyo umekuwa ukiongezeka. Leo hii kumesikika vilio vingi nchini vikilenga mazingira bora na fursa zaidi katika sekta ya elimu vinavyotokana na watu wengi kutambua nguvu ya elimu kwa vizazi vijavyo.
Wengi wenu ni mashahidi kuwa miongoni mwa changamoto kubwa ambayo watu wengi wajasiriamali wanaopenda kujiajiri wanakumbana nayo ni ukosefu wa mitaji na mikopo yenye masharti nafuu. Taasisi nyingi za fedha nchini na benki za biashara zinatoa mikopo kwa riba kubwa na masharti mengi, ambayo watu wengi hawawezi kuyamudu.
Kulingana na yakwimu za matokeo ya utafiti wa nguvukazi na ajira ya mwaka 2005/2006, zinaonesha kuwa watu milioni 2.3 walikuwa hawana Ajira. Idadi hiyo ni sawa na asilimia 5.8 ya watu wote nchini. Kwa upande wa Jiji la Dar es Salaam, asilimia 31.4 ya watu wenye uwezo wa kufanya kazi walikuwa hawana kazi.
Vilevile, kwa mujibu wa takwimu za hivi karibuni zinaonesha kuwa wastani wa nguvukazi hasa vijana wasomi wanaotafuta ajira kwa mwaka ni takriban laki nane hadi milioni moja. Hata hivyo, Ajira rasmi zinazopatikana nchini katika sekta ya umma na sekta binafsi ni kidogo, takriban ajira 80,000 hadi 100,000 kwa mwaka.
Pamoja na mafunzo ya ujasiriamali yanayotolewa, kwa vijana na wazee wanatakiwa kuwezeshwa na kuwekewa mifuko ya uwezeshaji yenye utaratibu maalum ulio wazi na mwepesi wa kupatikana kwa mikopo yenye riba nafuu kama vile inayobuniwa na mifuko ya sekta ya hifadhi ya jamii Tanzania
Na ndiyo maana mfuko wa mafao ya kustaafu GEPF kama mfuko wa hifadhi ya jamii umeamua kuwa na mkopo wa elimu "Kamata Madigrii na GEPF" kwa mwanachama yeyote aliyesajiriwa na mfuko wa mafao ya kuustaafu wa GEPF aliyeajiriwa katika sekta ya umma au binafsi na ambaye angependa kujiendeleza kielimu kuanzia ngazi ya cheti, diploma, shahada ya kwanza na ya pili mpaka shahada ya udaktari
Mwanachama wa GEPF anayetaka kukopa aina hii ya mkopo anatakiwa awe amepata nafasi katika chuo husika, awe ameruhusiwa na mwajiri kujiunga na masomo husika, awe amechangia katika mfuko kwa kipindi kisichopungua miaka miwili, na mwisho ni kwamba mwanachama anatakiwa kurejesha kupitia makato ya mshahara wake kwa kipindi cha kati ya miaka miwili mpaka miaka mitano.
Faida za mkopo huu wa elimu kwa wanachama wa GEPF ni kwamba wanapata fursa ya kuanza kunufaika na matunda ya uanachama wake akiwa kazini  na mwanachama kupata fursa ya mkopo wenye riba nafuu na masharti nafuu na kinga ya bima dhidi ya majanga
Utafiti unaonesha ya kuwa zaidi ya 1,000 ya wanachama wameanza kunufaika na huduma hii ya mkopo wa elimu na idadi kubwa ikiwa rika ya vijana nchini.

Mwandishi wa makala hii ni mwanzilishi wa Kituo cha HakiPensheni, mshauri na mtaalamu wa masuala ya pensheni. Kwa maelezo zaidi gayagmc@yahoo.com unaweza kutembelea tovuti hakipensheni monitor online na hakipensheni blog   +255 655 13 13 41

No comments :

Post a Comment