Naibu Waziri wa
Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mheshimiwa Elias Kwandikwa,
akiangalia namna watumishi wa mzani wa Tinde, mkoani Shinyanga wanavyopima na
kurekodi taarifa za magari yanaoingia kupima uzito kwenye mzani huo.
Naibu Waziri wa
Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mheshimiwa Elias Kwandikwa
(Mwenye suti), akiangalia namna shughuli za upimaji wa magari zinavyoendeshwa
katika mzani wa Tinde, mkoani Shinyanga. Kushoto kwake ni Meneja wa Wakala wa
Barabara (TANROADS), wa mkoa huo, Mhandisi Mibala Ndilindi.
Msimamizi wa shughuli
za mzani wa Tinde kutoka Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoani Shinyanga, Bw.
Lugembe Vicent (kushoto), akitoa taarifa ya kiutendaji ya mzani huo kwa Naibu
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mheshimiwa Elias
Kwandikwa. Mzani huo unapima magari 300 kwa siku.
Magari yakiwa katika
foleni kusubiri huduma za upimaji uzito ili kuendelea na safari kwenye mzani wa
Tinde, mkoani Shinyanga.
NA
WUUM, SHINYANGA
WAFANYAKAZI
wa mizani nchini wametakiwa kufanya kazi kwa weledi, uadilifu na kuachana na vitendo
vya rushwa ili kuleta tija na ufanisi wa kazi zao
katika usimamiaji na ulinzi wa barabara ambazo Serikali imekuwa ikitumia gharama kubwa katika ujenzi wake.
Hayo
yamesemwa na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi),
Mheshimiwa Elias Kwandikwa, leo mkoani Shinyanga, alipokuwa akikagua
mzani wa Tinde (Shinyanga), na Mwendakulima (Kahama), ambapo amesisitiza
ushirikiano kati ya wafanyakazi hao na madereva ili kutatua changamoto
zinazojitokeza katika vituo vya mizani.
katika usimamiaji na ulinzi wa barabara ambazo Serikali imekuwa ikitumia gharama kubwa katika ujenzi wake.





No comments :
Post a Comment