| Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Gerson Lwenge akizindua jengo jipya la Bodi ya Maji ya Bonde la Ziwa Tanganyika na Maabara ya Maji |
Waziri wa Maji na Umwagiliaji,
Mhandisi Gerson Lwenge akimkabidhi kitendea kazi Mwenyekiti w aBodi mpya
aliyoizindua ndugu Lister Kongola.
……………………..
Waziri wa Majina na Umwagiliaji,
Mhandisi Gerson Lwenge amezindua Bodi mpya ya Maji ya Bonde la Ziwa
Tanganyika
mkoani Kigoma Septemba 28, 2017 na kuitaka Bodi hiyo kusimamia matumizi
endelevu ya rasilimali za maji zilizopo ndani ya bonde hio kwa matumizi
endelevu.
“Bonde la Ziwa Tanganyika
ni bonde la tatu kwa ukubwa katika mabonde tisa yaliyopo nchini ambapo mabonde 7
ni shirikishi.
Alisema bonde hili ni shirikishi na nchi za DRC-Congo, Burundi, Rwanda
na Zambia.
"Asilimia 60 ya maji yanayoingia katika Ziwa Tanganyika
yanatoka Tanzania hivyo bonde hili kwa Tanzania
tunalitegemea sana." Alisema.
Mhandisi Lwenge alisema, sababu ya kuundwa kwa Bodi ni utekelezaji wa sheria ya Maji No. 11 ya Mwaka
2009 na Bodi itasimamia matumizi endelevu ya rasilimali za maji.
“Bodi hii ni muhimu sana kwa hiyo
kuteuliwa kwenu isiwe ni kwenda kupata posho tu na kutowajibika ipasavyo
bali ni kufanya kazi tunayoitegemea ya kukabiliana na changamoto
zinazowakabili wananchi”
alisemaWaziri.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi amesema bodi yake itatekeleza maagizo yote ya Mhe. Waziri.
No comments :
Post a Comment