Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza wakati wa
ufunguzi wa Mkutano wa Chama cha Majaji na Mahakimu kutoka nchi
wanachama wa Jumuiya ya Madola (CMJA) leo Jijini Dar es Salaam.
Kaulimbiu ya mkutano huo ni “Kujenga Mahakama shirikishi, inayowajibika
na thabiti kiutendaji”
Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof.
Ibrahim Juma akielezea jambo mbele ya washiriki wa mkutano wa wanachama
wa Chama cha Majaji na Mahakimu kutoka nchi za Jumuiya ya Madola (CMJA)
leo Jijini Dar es Salaam. Kaulimbiu ya mkutano huo ni “Kujenga Mahakama
shirikishi, inayowajibika na thabiti kiutendaji”
Rais wa Chama cha Majaji na
Mahakimu Tanzania Mhe. Jaji Ignas Kitusi akifafanua jambo mbele ya
washiriki wa mkutano wa Chama cha Majaji na Mahakimu kutoka nchi
wanachama wa Jumuiya ya Madola (CMJA) leo Jijini Dar es Salaam.
Kaulimbiu ya mkutano huo ni “Kujenga Mahakama shirikishi, inayowajibika
na thabiti kiutendaji”
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akifurahia jambo na Rais
wa Chama cha Majaji na Mahakimu kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya
Madola (CMJA) Jaji John Rounders wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa chama
hicho leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe.
Prof. Paramagamba Kabudi. Kaulimbiu ya mkutano huo ni “Kujenga Mahakama
shirikishi, inayowajibika na thabiti kiutendaji”
Kikundi cha sanaa kutoka shule ya
Sekondari Jitegemee wakituimbuza katika mkutano wa Chama cha Majaji na
Mahakimu kutoka nchi wanachama wa Jumuiya za Madola (CMJA) leo Jijini
Dar es Salaam. Kaulimbiu ya mkutano huo ni “Kujenga Mahakama shirikishi,
inayowajibika na thabiti kiutendaji”
Gavana wa Benki Kuu Tanzania Prof.
Benno Ndulu (wa kwanza kushoto) na Jaji Mkuu Mstaafu Mhe. Othman Chande
(wa pili) wpamoja na baadhi ya Majaji Wakuu kutoka nchi mbalimbali za
Jumuiya ya Madola akiwemo Jaji Mkuu wa Mahakama ya Juu ya Kenya Jaji
Francis Maraga (aliyekaa juu) wakifuatilia mkutano wa Chama cha Majaji
na Mahakimu kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola (CMJA) leo Jijini
Dar es Salaam. Kaulimbiu ya mkutano huo ni “Kujenga Mahakama
shirikishi, inayowajibika na thabiti kiutendaji”
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya
pamoja na baadhi ya washiriki wanawake wa Mkutano wa Chama cha Majaji na
Mahakimu kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola (CMJA) mara baada
ya kufungua mkutano huo leo Jijini Dar es Salaam. Kaulimbiu ya mkutano
huo ni “Kujenga Mahakama shirikishi, inayowajibika na thabiti
kiutendaji”
Picha na: Frank Shija – MAELEZO
…………………
Na.Paschal Dotto -Maelezo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mh.Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa serikali
inaendelea kuhakikisha Mahakama hazijihusishi na vitendo vya rushwa ili
kutoa haki kwa mujibu wa Sheria.
Mh. Samia ameyasema hayo Jijini
Dar es Salaam alipokuwa akifungua mkutano wa Chama cha majaji na
mahakimu wa nchi za Jumuiya ya Madola uliofanyika katika ukumbi wa Benki
Kuu ya Tanzania.
‘Ninaamini, nia ya kujenga
mahakama bora na yenye kuaminika kwa Tanzania haiwezi kutenganishwa na
juhudi za serikali katika kuondoa umaskini na rushwa” amesisitiza
Mh.Samia.
Aidha Makamu wa rais amesema kuwa
kuna uhitaji mkubwa kwa nchi kuwa na mahakama huru, makini na yenye
kuwajibika ipasavyo kwani mahakama huru ni msingi mzuri wa demokrasia.
Alisema kuwa pamoja na changamoto
mbalimbali za mahakama uhuru wa mahakama ambao ni umakini,uwajibikaji
na utoaji haki kwa kufuata utawala wa sheria kwa wananchi wake uko
palepale.
Kwa upande wa Tanzania Mhe. Samia
amesema kuwa katika awamu ya tatu ya mapambano dhidi ya rushwa ambapo
kwa awamu mbili zilizopita serikali imefanikiwa kwa kiasi kikubwa
kupunguza malalamiko yaliyotokana na ukiukwaji wa haki.
Katika awamu ya tatu ya mkakati wa
kupambana na rushwa utakaochukua miaka mitano kuanzia 2017 hadi 2022,
Tanzania itachukua uzoefu kutoka kwenye mkuatno huu wa kimataifa kutoka
kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya madola.
Kwa upande wake Jaji mkuu wa
Tanzania Professa Ibrahim Juma alisema mahakama hiyo iko huru na
inatekeleza majukumu yake pasipo kuingiliwa na mtu yeyote na akaahidi
kuendelea kubadilishana uzoefu na mahakama za nchi wanachama ili
kuboresha utendaji kazi.
Aidha Profesa Juma amesema
Mahakama ya Tanzania kupitia majaji imekubaliana kuwa kila Jaji
atatakiwa kuhukumu zaidi ya kesi 220 ambazo ni asilimia 38 ya kesi
zilizoahirishwa mwaka 2012 hadi asilimia 5 Desemba 2016 na hii
itafanyika kila mwaka ili kujipima wao wenyewe kama moja ya malengo
waliyojiwekea.
Akizungumzia mipango ya mahakama
hiyo Profesa Juma amesema kuwa hadi kufikia mwaka 2020 mahakama hiyo
itakuwa imekamilisha ujenzi wa mahakama Kuu 13,mahakama za hakimu mkazi
14,mahakama za Wilaya 48,pamoja na mahakama za Mwanzo 100.
Mkutano wa mwaka huu wa chama cha
majaji na mahakimu wa nchi za jumuiya ya madola umefanyika kwa mara ya
kwanza hapa nchini tangu Tanzania ijiunge na chama hicho mwaka 1970.
No comments :
Post a Comment