Waziri
wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama
(Mb) akiwa kwenye mazungumzo na Mwakilishi Mkazi UNICEF Tanzania Bi. Maniza Zaman,
(kushoto), Ofisini kwake jijini Dar es Salaam, Agosti 3, 2017. Mazungumzo hayo
yalijikita katika uboreshaji wa huduma za watoto nchini.
NA OWM,
DAR ES SALAAM
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Mb) Jenista
Mhagama akutana na kufanya mazungumzo na Mwakilishi Mkazi wa UNICEF Tanzania
Ms. Maniza Zaman Ofisini kwake na kuzungumzia masuala mtambuka juu ya kuboresha
huduma za watoto Jijini Dar es Salaam Agosti 3, 2017.
Waziri Jenista pamoja na masuala mengine amelishukuru
Shirika la Umoja wa Mataifa (UNICEF) kwa kushirikiana na Serikali ya Awamu ya
Tano katika utekelezaji wa Programu ya Kitaifa ya Masuala ya Kijamii (National
Frame -work Social Protection) na mapitio ya utengenezaji wa Sera ya Hifadhi ya
Jamii (Social Security Policy) na kueleza kuwa Serikali imeguswa na jitihada za
UNICEF kwa kuunga mkono jitihada za serikali katika Nyanja hii.
Ms. Maniza amesema “UNICEF ina mipango mbalimbali
inayotaka kutekeleza kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania mipango hiyo ni
pamoja na kuboresha masuala ya Elimu kwa watoto, Masuala ya Lishe, Watu Wenye
Ulemavu, UKIMWI kwani huduma hizi ni za msingi hivyo UNICEF itaangalia
namna ya kutekeleza mipango hii kwa Tanzania”.
“Tumeweza kuandaa makongamano na majukwaa ya wahariri
kutoa elimu kupitia Vyombo vya Habari, Viongozi wa Dini kuhusu masuala ya
watoto nchini Uganda na Brazil ambayo imefanikiwa kwa asilimia 80 hivyo
tunaamini Tanzania pia inaweza kuanzisha majukwaa kama hayo katika kuboresha
masuala ya watoto hapa nchi kwa kushirikiana na UNICEF” alisisitiza Ms. Maniza.
Jenista amemuahidi Mwakilishi Mkazi Ms. Maniza kuandaa
mazungumzo ya pamoja kwa kushirikiana na Wizara na sekta nyingine ili kuweza
kuzungumzia masuala ya watoto na masuala mengine mtambuka kwa ajili ya kuleta
mabadiliko na kuboresha masuala ya watoto hapa nchini.
No comments :
Post a Comment