Thursday, August 3, 2017

UHAMIAJI YAMSAFISHA WALLACE KARIA KUHUSU UTATA WA URAIA WAKE. NI YULE MGOMBEA URAIS WA TFF


Bw. Wallace John Karia,Mgombea nafasi ya Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, (TFF).
Michuzi Karia
Msemaji Mkuu wa Idara ya Uhamiaji, Mrakibu wa Uhamiaji Ally Mtanda akiongea na Vyombo vya Habari kuhusu matokeo ya uchunguzi wa suala la utata wa uraia wa Bw. Wallace John Karia, ambaye ni mgombea wa nafasi ya Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, (TFF). Kutokana na pingamizi lililowekwa na Wakili Imani Madega, mgombea mwingine wa nafasi hiyo, akilalamika kuwa uraia wa Bw. Karia una utata. Kwa matokeo hayo Karia sasa yuko huru kuwania nafasi hiyo.

No comments :

Post a Comment