Wednesday, August 16, 2017

MWANARIADHA ALPHONCE SIMBU APOKELEWA KWA SHANGWE NCHINI


PICHA 3
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo, Mhe.Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) pamoja na baadhi ya Viongozi wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) akipoka bendera ya Taifa toka kwa Wanariadha Aphonce Simbu na wenzake baada ya kuwasili toka nchini Uingereza kwenye Mashindano ya Marathon ya 2017.
PICHA 4
Mwanariadha Alphonce Simbu akiwashukuru Viongozi mbalimbali waliokuja kumpokea na kumpongeza kwa ushindi wake katika Mashindano ya Mbio nchini Uingereza kwa mwaka 2017 ambapo aliweza kujinyakulia medali ya shaba.
PICHA 5
Wazazi wa Mwanariadha Alphonce Simbu wakiwaonyesha Waandishi wa habari (hawapo pichani) medali ya shaba aliyoshinda mtoto wao katika Mashindano ya Mbio nchini Uingereza kwa mwaka 2017.
PIX 1
Mwanariadha Alphonce Simbu akiwaonyesha Waandishi wa habari (hawapo pichani) medali ya shaba aliyoshinda katika Mashindano ya Mbio nchini Uingereza kwa mwaka 2017.
04
Simbu akipokelewa na mashabiki wake akiwa amembeba mtoto wake

Simbu alifanikiwa kumaliza katika nafasi ya tatu nyuma ya Tamirat Tola (Ethiopia) aliyemaliza nafasi ya pili na Geoffrey Kirui (Kenya) aliyeibuka mshindi wa mashindano hayo kwa upande wa wanaume.
Waziri Mwakyembe amewapongeza wanariadha wote waliokwenda London kuiwakilisha Tanzania na kufanikiwa kurudi na medali.

………………..
MSHINDI wa tatu wa Mbio za Dunia za London Marathon mwaka huu, Felix Simbu amesema kuwa ushindi huo alioupata si wapeke yake bali wa wanariadha wote ambao walienda kushiriki kutokana walijitoa muhanga hadi kufanya vizuri.
Simbu alishika nafasi ya tatu katika mbio za Km 42 na kuitoa kimasomaso Tanzania ambayo ...ilikuwa haijafanya vizuri katika mashindano hayo kwa miaka mingi.
Akizingumza na Mtandao huu wa www.Fullshangweblog.com,  baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa akitokea nchini Uingereza na kupokelewa na mamia ya mashabiki, Simbu alisema haikuwa kazi rahisi kupata medali hiyo imetokana na wao kujitoa muhanga.
“Ushindi huu si wangu peke yangu bali ni wa wetu sote kutokana tulikuwa na umoja.”Huu ni ushindi wa wote, hivyo umoja wetu utazidi kujitahidi kufanya vizuri zaidi hapo baadae,” alisema.
Alisema, aliona kama maajabu kwa ushindi huo baada ya kuona bendera ya Tanzania inapandishwa kuashiria ushindi wake.Awali, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Harryson Mwakyembe alisema ushindi huo umewafanya Watanzania wawe na furaha kutokana hawakuwa na imani ya kufanya vizuri.
Alisema ni wakati sasa wa kuwekeza katika mchezo huo ili uweze kupiga hatua zaidi. Simbu aliwasilia saa 12:20 jioni kutokana na kuchelewa kufika ambapo awali aliyatarajiwa kufika saa 6:05 mchana.
Kufika kwake alipokelewa na vikundi mbalimbali vya ngoma, wasanii ambao waliongozwa Khadija Kopa na Riyama Ally.

No comments :

Post a Comment