Na Tiganya Vincent
Urambo
16.8.2017
WALENGWA wa Mpango wa Kunusuru
kaya maskini wametakiwa kuhakikisha wanatimiza masharti ya elimu na afya
ili kuepuka kukwata fedha ambazo wanastahili kupata kutoka Mfuko wa
Maendeleo ya Jamii(TASAF) kwa ajili ya kuwahuduma watoto wao.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Afisa
Uhawilishaji Fedha kwa njia ya ...
Mtandao wa TASAF Bibi Kweji Kasulende
wakati akijibu malalamiko kutoka kwa wakazi wa maeneo mbalimbali
Wilayani Urambo , ambao wamepata adhabu ya kukwata fedha zao kwa
sababu ya kukosekana taarifa zinazoonyesha kuwa waliwapeleka watoto wao
Kliniki na wengine wanahudhuria shule bila kukosa
Alisema kuwa baadhi ya walengwa
wamekuta wakipata pesa pungufu kwa sababu ya kukosekana taarifa
zinaonyesha kuwa wamekuwa kila mwezi hawapeleki watoto wao kupata huduma
za Kliniki kama inavyotakiwa.
Bibi Kasulende aliongeza wengine
wamekuwa wakikatwa fedha kwa sababu ya watoto wao kutohudhuria shule au
wakati mwingine majina waliwaandikisha Shuleni kuwa tofauti na yale
yalipo katika Mpango wa TASAF.
Alisisitiza umuhimu wa walengwa
kuhakikisha taarifa zilizopo TASAF zinawiana na zile za Shule na vile
vile kuhakikisha kuwa wanapowapeleka watoto wao Kliniki taarifa ya
mahudhurio zinaonekana katika kumbukumbu za Mfuko huo ili kuwaondolea
usumbufu usio wa lazima.
“Ili kuondoa malalamiko hayo ni
vema walezi au wazazi wa watoto mkahakikisha mnawapeka Kliniki watoto
wenu walio chini ya miaka mitano … na wale wanaosoma waende Shule bila
kukosa na kufuatilia mahudhurio yao siku zote za masomo” alisisitiza
Kasulunde.
Bibi Kasulende alisema hatua hiyo
itasaidia kuaondoa usumbufu ambao wamekuwa wakiupata kutokana na kukatwa
fedha kwa sababu ya wao kushindwa kabisa kurekebisha taarifa zao
zinahusua masuala ya elimu na mahudhurio ya Kliniki ya watoto wao.
Kwa upande wa Mratibu wa TASAF
Mkoani Tabora Bw. Ngoko Buka aliwatoa hofu walengwa wote wa mpango huo
ambao wamekatwa fedha zao kwa sababu ya kushindwa kurekebisha taarifa za
watoto na kuwaeliza kuwa wakishazifanyia marekebisho fedha yao
zitalipwa katika awamu ijayo.
Aliwataka kutumia wajumbe wa
Kamati za Jamii za Utekelezaji wa Mpango(CMC) kuhakikisha wanawasaidia
Walengwa kurekebisha kasoro zilizopelekea wao kukatwa fedha ambazo
kimsingi walipaswa walipwe.
Bw. Buka aliwaomba walengwa
kuhakikisha kila mtoto anapotoka hatua moja kwenda nyingine wanapeleka
taarifa katika Ofisi husika ili kuepuka makosa ya aina hiyo kujirudia
tena na kujikuta wakipata pesa pungufu.
Katika hatua nyingine baadhi ya
walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikimi wameishukuru TASAF kwa
kuwawezesha kifedha jambo lililowasaidia kusomesha watoto wao na
kuwahudumia katika masula ya sare na kodi za Hosteli,
Mmoja wa Walengwa hao Bibi Yasinta
Emmanuel alisema kuwa fedha hizo zimemsaidia katika kusomesha watoto
wake wawili Shule ya Msingi na kuanzisha mradi mdogo wa ufugaji wa kuku
na ununuzi wa mabati sita kwa ajili kuezekea nyumba yake.
Mlengwa mwingine Mohamed Juma
alisema kuwa fedha alizozipokea kutoka TASAF chini ya Mpango wa
Kunusuru Kaya Masikini zimemsaidia kuanzisha mradi wa ufugaji wa nyuki
kwa ajili ya uzalishaji wa asali.
Alisema kuwa hadi hivi sasa anayo mizinga 19ambapo kati ya hiyo 9 ni ya kisasa na iliyobaki ni ile ya kienyeji.
No comments :
Post a Comment