Wednesday, May 31, 2017

ZAMBIA YAIFUNGA UJERUMANI NA KUTINGA ROBO FAINALI

Mabingwa wa Afrika Zambia wametokea nyuma na kuifunga Ujerumani kwa magoli 4-3 katika muda wa ziada na kutinga robo fainali ya Kombe la Dunia U20 Korea Kusini.

Zambia ilionekana kama imeshinda mechi hiyo ikiwa inaongoza kwa magoli 3-1 katika dakika ya 89, lakini magoli ya Suat Serdar na Jonas Arweiler yalifanya ngoma kuwa sare.

Katika mchezo huo shujaa alikuwa ni Shemmy Mayembe kwa kuifungia Zambia goli la mapema katika kipindi cha pili cha dakika 30 za ziada.
Kwa matokeo hayo Zambia sasa watavaana na Ufaransa ama Italia katika hatua ya nane bora siku ya jumatatu.

No comments :

Post a Comment