Wednesday, May 10, 2017

PROFESA MBARAWA AELEKEA KIGALI RWANDA, KUMWAKILISHA RAIS MAGUFUL KWENYE MKUTANO WA MASUALA YA ICTI



WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, ameondoka nchini leo Mei 10, 2017 kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwenye mkutano wa siku mbili wa “Transform Africa Summit 2017” ulioanza leo Mei 10, 2017  mjini Kigali, Rwanda.
Taarifa kutoka ofisi yake zimesema mkutano huo utawakutanisha viongozi na wataalam mbalimbali barani Afrika kwa lengo la kujadili masuala kadhaa ikiwemo maendeleo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT), hususan katika ukanda wa Afrika Mashariki.
Katika mkutano huo, Profesa Mbarawa ataeleza kwa kina changamoto na mafanikio yaliyofikiwa na Tanzania katika uwekezaji wa Miundombinu ya Habari na Mawasiliano, Maendeleo ya Sera na Miongozo inayotumika hapa nchini katika kusimamia sekta hiyo kwa lengo la kukuza uchumi wa nchi na kuiunganisha Tanzania na Mataifa mengine. pichani chini Rais wa Rwanda, Paul Kagame akifungua mkutano huo ambao ulikwenda sambamba na maonesho ya kiteknolojia.
Rais wa Rwanda Paul Kagame, akitoa hotuba ya ufunguzi wa mkutano wa siku mbili wa “Transform Africa Summit 2017” ulioanza leo Mei 10, 2017  mjini Kigali, Rwanda.
Washiriki wa mkutano huo wakisikiliza hotuba ya Rais Kagame wakati wa ufunguzi leo

No comments :

Post a Comment