Na Mahmoud Ahmad Kondoa
Sakata la wachimbaji wadogo wa
madini na Kampuni ya Kidee Minningi limechukuwa sura mpya baada ya
Mwenyekiti wa kijiji cha Changaa Kenyata Athman Kukiri kampuni hiyo
kukiuka makubaliano ya mkutano mkuu wa wananchi wa kijiji hicho.
Akizungumza baada ya uongozi wa
kumucha kufika ofisini kwake kwenda kuomba PML za
kikundi
zilizohifadhiwa ofisini hapo mwenyekiti huyo alisema kuwa ni kweli
makubaliano yao ya kukisaidia kikundi hicho ili kiweze kupata leseni
yamekiukwa na kampuni hiyo kwa kutangulia kuja na leseni kabla ya
mkutano mkuu haujakaa.
Athman alisema kuwa kwenye mkutano
mkuu wa kijiji na mwekezaji huyo atakisaidia kikundi hicho kupata
leseni jambo ambalo hajalitekeleza hadi leo tunavyoongea pia aliahidi
kukisaidia kikundi kuwepo kisheria nay eye ndio amekuwa wa mwanzo
kutonyesha ushirikiano alioahidi mbele ya mkutano wa wananchi.
“Suala hili ni kweli nilifikisha
katika mkutano mkuu wa kijiji ili muwekezaji apate Baraka za kupata
muhtasari lakini kikundi cha KUMUCHA kilihoji uhalali wa muwekezaji
kuanza kazi eneo ambalo vijana walishaanza kazi za uchimbaji mdogo na
ndipo alipoandikia ofisi ya kijiji barua ya kulalamika kuvamiwa na
mwekezaji,na ndipo mwekezaji akiwakilishwa na meneja wake Ismail Kidee
alisema anakitambua kikundi na watashirikiana nao jambo ambalo
halikutimizwa na kampuni hiyo”alisema Athman.
Hata hivyo wanakikundi
hawakuridhishwa na majibu hayo ndipo wakatoa katiba yao isomwe hadharani
ili wananchi watambue haki zao za msingi jambo ambalo meneja wa kidee
alikiri kuwa hiki ni kikundi kinachostahili kushirikiana nacho jambo
lilipingwa vikali na KUMUCHA kwa misingi nao waliwasilisha mbele ya
mkutano huo maopmbi ya muhtasari wa kuomba leseni.
Baada ya mkutano huo matarajio ya
kikundi hicho ni kupewa muhtasari lakini kutokana na kauli ya mwekezaji
kwenye ofisi ya kijiji ni kuwa yeye ni mwenye dhamana ya kikundi na siyo
wao kupewa leseni bila kujali wao ndio waanzilishi wa shughuli za
uchimbaji kupitia PML walizopewa na wizara ya madini.
Akizungumza mara baada ya kufika
ofisi ya kijiji cha Changaa Mwenyekiti wa kikundi cha KUMUCHA Donmilaan
Shirima alisema kuwa baada ya mwekezaji kufikisha vitendeakazi vyake
eneo husika walitumia migambo wa kijiji kuwa ndio walinzi wa eneo la
mgodi kupitia serikali ya kijiji jambo ambalo lilitufanya kuiandikia
barua serikali ya kijiji bkutoa taarifa za uvamizi wa mwekezaji huyo.
Amesema kuwa cha kushangaza hatua
ya barua yetu haikufanyiwakazi na badala yake muhtasari alipewa
muwekezaji na sisi kuachwa kuwa ni watumwa kwenye eneo letu,sisi
tukabakia na mashangao wa kutoheshimiwa kwa kikundi ambacho
kinatambuliwa kisheria.
“Unajua suala hili limekuwa
likitushangaza kwa mamlaka za serikali kutoa eneo mmoja kwa watu wawili
ambapo kikundi kilipewa PML halafu anakuja mwekezaji na leseni kwenye
eneo hilo kabla ya mkutano mkuu kumpa ridhaa ya umiliki wa eneo jambo
linalotia shaka utendeji wa mamlaka za serikali za vijiji na wizara
husika”alisema shirima
Hata hivyo ofisa wa madini mkoa wa
Dodoma (RMO)hadi sasa haijatuita kwenye mazungumzo ambayo kamishna
msaidizi wa madini kanda ya kati alituahidi kushirikishwa kwenye kikao
cha mwekezaji na kampuni ya milenium builders japo kikao hicho
kimeshafanyika kwa awamu ya kwanza bila kumucha kushirikishwa
No comments :
Post a Comment