Thursday, April 20, 2017

MKANDARASI AANZA KAZI USAMBAZAJI MAJI PEMBEZONI MWA BOMBA KUU RUVU JUU.


indexNa Daudi Manongi-MAELEZO.
Wizara ya Maji na Umwagiliaji imesema kuwa mkandarasi  ameanza kazi ya ujenzi wa mabomba ya usambazaji katika maeneo ya Malamba Mawili,Msigani,Mbezi Luisi,Msakuzi,Kibamba,,Kiluvya,Mloganzila na Mailimoja na atakamilisha kazi hiyo mwaka huu 2017.
Hayo yamesemwa leo Bungeni Mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji
Mhe.Isack Kamwelwe wakati akijibu hoja mbalimbalia za wabunge.
“Baada ya kukamilika kwa mradi maeneo mengi ndani ya kilomita 12 ya pembezoni mwa  bomba kuu la Ruvu Juu yameanza kupata huduma ya Maji”,Aliongeza Mhe.Kamwelwe.
Amesema kuwa maeneo ambayo yanapata maji kwa sasa kutoka Bomba la Ruvu Juu ni pamoja na Mlandizi na vitongoji vyake, Visiga, Misugusugu, Soga, Korogwe, Picha ya Ndege, Kwa Matiasi,Tumbi, Mailimoja, Pangani, Kiluvya, Kibamba, Mloganzila, Mbezi kwa Yusufu,Mbezi Mwisho, Kimara, Mavurunza, Baruti, Kibo, Kibangu,Tabata, Segerea, Kinyerezi na Karakata.
Aidha maeneo ambayo  bado hayajaanza kupata huduma ya maji yatapata huduma hiyo baada ya utekelezaji wa miradi mipya ya kujenga mtambo wa mabomba ya kusambaza maji katika maeneo yote ambayo hayana huduma hiyo, Amesema kuwa miradi hii itatekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha .

No comments :

Post a Comment