Friday, April 14, 2017

Kampuni Ya Mobisol Yazindua Kampeni Ya ‘Hamasika Na Masika’


unnamed
Bidhaa zinazotumika umeme wa jua zinazosambazwa na Mobisol Tanzania
A 1
Wafanyakazi wa Mobisol wakionyesha  baadhi yabidhaa za kampuni katika promosheni iliyofanyika hivi karibuni
A
Chaji za sola za Mobisol
…………..
 
Kampuni ya Kijerumani ya Mobisol inayosambaza nishati ya umeme wa jua na vifaa imara na vya kisasa vinavyotumia nishati hiyo  nchini  imezindua kampeni maalumu ya kuhamasisha wananchi    kujiunga na mtandao wake inayojulikana kama “Hamasika na Masika”.
Kupitia kampeni hii wateja watakaonunua mitambo ya umeme wa nishati ya jua katika kipindi cha mwezi huu mwa Aprili na Mei wataingia kwenye droo na kuweza kujishindia pikipiki aina ya Boxer na pia zaidi ya shilingi milioni 4 zimetengwa wa ajili ya kutoa zawadi za fedha taslimu kwa washindi ambapo pia wateja wa sasa wa Mobisol watakaoshawishi  wateja wapya kujiunga na mtandao wa Mobisol nao watashirikishwa na droo ya kwanza itafanyika wiki hii.
Meneja Chapa wa Mobisol Tanzania, Seth Mathemu anasema “Tunataka wateja wetu waweze kunufaika zaidi katika kipindi hiki kwa kuweza kujishindia zawadi mbalimbali pale wanaponunua mtambo wao wa Mobisol. Ni utamaduni wetu kugawana sehemu ya faida yetu na wateja wanaoifanya Mobisol kuwa kampuni bora ya sola katika ukanda wa Afrika mashariki
Matheme alisema Shindano hili linawajumuisha wakazi wote wa mikoa zaidi ya ishirini Tanzania bara ambapo Mobisol inatoa huduma zake na kuitaja mikoa hiyo kuwa ni Arusha, Kilimanjaro, Manyara, Singida, Dodoma, Tabora, Shinyanga, Mwanza, Mara, Kagera, Simiyu, Geita, Kigoma, Rukwa, Iringa, Mbeya, Songwe, Njombe,  Pwani pamoja na Morogoro.
Aliongeza kusema kuwa  kampuni ya Mobisol inauza na kufunga, mitambo ya bora ya Sola nchini pamoja na vifaa  vya matumizi ya nishati hii ambavyo ni  Paneli ya Sola, betri, taa, Televisheni, Radio, Tochi, Mashine ya Kunyolea nywele, MobiCharger (Kifaa cha kuchajia Simu) na Friji.
Wakati ni huu kwa watanzania kupata nishati bora ya umeme wa jua na vifaa vya kisasa na natoa wito kwa wananchi kuchangamkia fursa hii  kujiunga na  familia ya Mobisol waweze kuishi maisha ya kisasa  na kujishindia zawadi kupitia kampeni hii ya ‘Hamasika na Masika’.Kwa maelezo zaidi ya kupata huduma za Mobisol mteja anaweza kupiga simu namba 0800 755 000 bure na utahudumiwa.Alisema

No comments :

Post a Comment