Mhe.
Mahiga akiwakilisha Ujumbe Maalum wa Mhe. Rais Magufuli kwa Bi Maria
Luiza Ribeiro – Mnadhimu Mkuu wa Ofisi ya Katibu Mkuu wa Umoja wa
Mataifa.
Mhe. Mahiga akielezea ujumbe aliouwasilisha kutoka kutoka kwa Rais Magufuli. (Kushoto
kwa Mhe. Mahiga ni Balozi Celestine Mushy Mkurugenzi Idara ya
Ushirikiano wa Kimataifa, kulia ni Mhe. Balozi Modest Mero – Mwakilishi
wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa na mwisho ni Lt Col
George Itang’are – Mwambata Jeshi.
Mhe. Mahiga akizungumza na Mabalozi wa nchi za SADC wanaochangia majeshi ya Ulinzi wa Amani – FIB – MONUSCO – DRC.
Mhe. akiagana na Bi Ribeiro baada ya Mazungumzo
………………………………………………………………………………
Mhe. Dkt Augustine Mahiga
amewasilisha kwenye Umoja wa Mataifa ujumbe maalumu wa Mhe. John Pombe
Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti
wa Asasi ya SADC ya Siasa, Ulinzi na Usalama unaoeleza msimamo wa Wakuu
wa
Nchi na Serikali ya Nchi za SADC kuhusu kuongezewa muda wa jukumu wa
kikosi cha Ulinzi wa Amani cha Umoja wa Mataifa (MONUSCO – Force
Intervention Brigade – FIB) nchini DRC kinachotarajiwa kumaliza muda
wake wa jukumu ifikapo tarehe 31 Machi 2017.
Waziri Mahiga aliwasilisha ujumbe
huo kwa Mhe. Maria Luiza Ribeiro, Mnadhimu Mkuu wa Ofisi ya Katibu Mkuu
wa Umoja wa Mataifa (Chef de Cabinet) kwa niaba ya Mhe. Antonio
Guterres, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ambaye alikuwa safarini nje ya
Marekani kikazi.
Akiwasilisha ujumbe huo, Mhe.
Mahiga alieleza kuwa, moja ya maazimio ya Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa
Nchi na Serikali wa SADC uliofanyika tarehe 18 Machi 2017 nchini
Swaziland ni pamoja na Jumuiya ya SADC kufikisha ujumbe kwenye Umoja wa
Mataifa wa kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Umoja wa Mataifa
(Baraza la Usalama) kukiongezea muda kikosi cha Ulinzi wa Amani cha
Umoja wa Mataifa kinachotarajia kumaliza muda wake wa jukumu kwa
mujibu wa Mkataba tarehe ifikapo 31 Machi 2017.
Mhe. Mahiga alimueleza Bibi Maria
kuwa, Jumuiya ya SADC inaupongeza Umoja wa Mataifa kwa jitihada za
kuleta amani nchini DRC na kwamba, Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC
wanamatumaini kuwa kuongezewa muda kwa kikosi hicho kutazingatia
mahitaji ya changamoto za usalama zilizopo nchini DRC na hivyo
kukiwezesha kikosi hicho kukabiliana na changamoto hizo.
Mhe. Mahiga alitumia nafasi hiyo
kueleza hali iliyopo kwa sasa ya ulinzi na usalama katika nchi za
Ukanda wa Maziwa Makuu, ambapo aligusia na kuomba Umoja wa Mataifa
kuongeza jitihada za kupatia ufumbuzi wa matatizo yaliyopo nchini DRC na
Burundi.
Waziri Mahiga alifanya mazungumzo
na wadau mbalimbali ikiwa ni pamoja na Mabalozi wa Nchi zinazochangia
vikosi vya Ulinzi na Usalama MONUSCO – FIB nchini DRC, Balozi wa
Uingereza kwenye Umoja wa Mataifa ambaye ni Rais wa Baraza la Usalama la
Umoja wa Mataifa, Balozi wa Ufaransa kwenye Umoja wa Mataifa
(Pen-holder) wa DRC na Mabalozi wa Afrika wanaowakilisha nchi zao kwenye
Umoja wa Mataifa.
Mhe. Mahiga anatarajia kuhutubia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kesho tarehe 30 Machi 2017.
No comments :
Post a Comment