Katibu Mkuu Sekta ya Viwanda,
Wizara ya Viwanda Biashara na Uwekezaji Dkt. Adelhelm Meru akifungua
warsha ya siku moja ya tathmini ya Sera ya Maendeleo ya Viwanda Vidogo
na Biashara Ndogo iliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Sekta ya Viwanda,
Wizara ya Viwanda Biashara na Uwekezaji Dkt. Adelhelm Meru (kulia)
akiteta jambo na Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Viwanda Vidogo na Biashara
Ndogo Bw. Boniface Michael.
Mwenyekiti Asasi ya Mikono
Cultural Heritage Bw. Henry Orauya akieleza jambo kwa Katibu Mkuu Sekta
ya Viwanda, Wizara ya Viwanda Biashara na Uwekezaji Dkt. Adelhelm Meru,
mara baada ya ufunguzi wa warsha ya tathmini ya Sera ya Maendeleo ya
Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo iliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo
Bw. Boniface Michael.
Katibu Mkuu Sekta ya Viwanda,
Wizara ya Viwanda Biashara na Uwekezaji Dkt. Adelhelm Meru akiwa kwenye
picha ya pamoja na wadau wa warsha ya tathmini ya Sera ya Maendeleo ya
Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo iliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
Mratibu wa Masuala ya Ukimwi
nchini toka Shirika la Kazi Duniani (ILO) Bibi. Getrude Sima akisisitiza
jambo kwa Katibu Mkuu Sekta ya Viwanda, Wizara ya Viwanda Biashara na
Uwekezaji Dkt. Adelhelm Meru mara baada ya ufunguzi wa warsha ya
tathmini ya Sera ya Maendeleo ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo
iliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
(Picha na Frank Mvungi-MAELEZO)
……………..
Na Fatma Salum-MAELEZO
Serikali kupitia Wizara ya Viwanda Biashara na Uwekezaji inaendelea kufanya maboresho ya sekta ya viwanda ili kuendana na kasi ya ujenzi wa uchumi wa viwanda hapa nchini.
Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu
Sekta ya Viwanda, Wizara ya Viwanda Biashara na
Uwekezaji Dkt. Adelhelm
Meru wakati akifungua warsha ya siku moja ya tathmini ya Sera ya
Maendeleo ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo iliyofanyika leo Jijini
Dar es Salaam.
Dkt. Meru alieleza kuwa lengo la
kufanya tathmini hiyo ni kuboresha mazingira ya uwekezaji kwenye viwanda
vidogo na vya kati kwa kuwa kuna mabadiliko mengi yamefanyika tangu
sera hiyo ianze kutumika mwaka 2003.
“Viwanda hivyo vinachangia
asilimia 27 ya pato la taifa hivyo ni muhimu kupitia upya sera hii na
kupata maoni ya wadau kwani hivi sasa kuna mabadiliko mengi ya
teknolojia, sheria na taratibu za uwekezaji.” Alisisitiza Dkt. Meru.
Aidha alisema kuwa Serikali
itafungua dirisha dogo kwenye Benki ya Uwekezaji (TIB) kwa ajili ya
kuwasaidia wawekezaji wa viwanda vidogo na vya kati kupata mitaji ya
kuanzisha na kuendeleza viwanda vyao.
Akieleza mipango ya baadae Dkt.
Meru alibainisha kuwa Serikali ina mpango wa kuanzisha Benki ya
Maendeleo ya Viwanda itakayowawezesha wazawa na wawekezaji wengine
kupata mitaji yenye riba na masharti nafuu ili kuchochea ukuaji wa sekta
hiyo.
Dkt. Meru alitoa wito kwa
Watanzania kujikita kwenye uwekezaji wa viwanda kwa kuwa ndio njia pekee
ya kukuza uchumi kwa haraka na kuongeza ajira, teknolojia, biashara na
mitaji.
Tathmini ya Sera ya Maendeleo ya
Viwanda imekusudiwa kutoa mwelekeo wa namna bora ya kujikita kwenye
uchumi wa viwanda kupitia uwekezaji wa viwanda vidogo na vya kati.
No comments :
Post a Comment