Sunday, March 26, 2017

SAKATA LA MACHIMBO YA DHAHABU TUMBELO MCHIMBAJI ASHIKILIWA NA POLISI


indexNa Mahmoud Ahmad Kondoa
Mmiliki wa kampuni ya Kidee Minning na polisi wilayani Kondoa wamekuwa wakiwakamata wachimbaji wadogo na kuwabambikia kesi ili kuwatisha waondoke kwenye eneo la machimbo ya dhahabu yaliopo kwenye Mtaa wa Tumbelo licha ya suala hilo kuwepo kwenye mamlaka za
serikali wilayani humo.
Hadi sasa mmoja wa wachimbaji hao anazuiliwa kituo cha polisi wilayani Kondoa huku akibambikiwa kesi ya Madawa ya kulevya na polisi waliomkamata eneo la Kondoa mjini kwa madai waliambiwa eneo hilo kunalimwa madawa ya kulevya hali hiyo imetokana na wiki iliyopita kwa wachimbaji wawili kukamatwa.
Aidha imeonekana mmiliki wa Kampuni hiyo amekuwa akiwatumia polisi kuendelea kuhakikisha anafanikiwa kuwadhibiti wachimbaji hao na kulitwaa eneo wanalochimba madini ya dhahabu katika Mtaa wa changaa licha ya suala hilo kuwapo kwenye mamlaka za serikali zikishughulikia suala la leseni na mmiliki halali.
Sakata la Maombi ya Leseni kwa wachimbaji wadogo wa madini kwenye eneo la Kata ya Changaa wilayani Kondoa limegubikwa na sintofahamu kwa leseni kutolewa kinyume na taratibu za utoaji wa leseni na kuwaacha waliomba leseni kwa mda mrefu.
Hatua hiyo imeonekana kwenye Ofisi ya Madini Kanda ya Kati kutofika eneo la uchimbaji na kujiridhisha ambapo kuna makundi matatu yaliomba leseni na kutoa kwa kampuni mmoja bila kufuata taratibu hali inayoleta sintofaham kwa walikuwa eneo hilo wakiendelea na uchimbaji
kwa kampuni ya kidee Minning hali iliyopelekea wachimbaji na kampuni nyingine zilizotangulia kwenye mchakato wa uombaji wa leseni kuachwa na kupewa kampuni hiyo.
Sakata hilo hadi sasa mamlaka husika zimebakia na kigugumizi cha kuongea hatima ya wachimbaji wadogo  hao wenye kikundi cha KUMUCHA Changaa kinachotambuliwa na serikali ya wilaya na huku wakiwa na pmo ya awali ya umiliki wa eneo hilo.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mkoani singida Kamishna msaidizi wa madini kanda ya kati Sostenes Msola ameahidi kulifuatilia suala hilo kwa ukaribu ambapo pia ataandikia ofisi yake iliyoko Dodoma kulifuatilia suala hilo.
Msola amesema kuwa licha ya ofisi yake ya Dodoma kuonekana kutoa leseni bila ya kujiridhisha kufika eneo la machimbo lakini kampuni hiyo ina leseni teyari hivyo ipo kisheria japo kuna mazingira ambayo hayakuyafuata taratibu za kisheria.
Amesema kuwa suluhu ya jambo hilo ni kukaa kwenye meza ya mazungumzo kulijadili kwa kuwaleta wote wenye malalamiko mezani kwani hata hawa wachimbaji wadogo wana mashiko kwenye suala hili kwani nia ya serikali ni kuona wachimbaji hao wanaendelezwa.
Nae Mmiliki wa Kampuni ya Kidee minning  Hassan Kidee alipotafutwa kwa njia ya simu kujibu tuhuma hizo alidai yeye hana shida na wachimbaji hao wanaoendelea na uchimbaji na waendelee na majukumu yao ila wafuate utaratibu  wa uchimbaji.
Kidee amesema kuwa kijana mchimbaji aliekamatwa na kwa kosa la kumtishia mwenyekiti wa  serikali ya mtaa wa tumbelo ila yeye alishiriki kuhakikisha kijana huyo anapatikana ili kuondoa sifa mbaya kwa wachimbaji hao.

No comments :

Post a Comment