Dkt. Bingwa wa Upasuaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Ibrahim
Mkoma akiwaeleza waandishi wa habari huduma ya matibabu waliokua
wakimpatia Neema Mwita Wambura tangu kufikishwa hospitalini hapo.
Dkt.
Mkoma akionyesha baadhi ya sehemu ambazo Neema amefanyiwa upasuaji
baada ya kupata majeraha makubwa baada ya kumwagiwa maji ya moto na mume
wake huko mkoani Mara.
Neema
Mwita akimshukuru Rais Dkt. John Magufuli pamoja na wa watoa huduma
wa Hospitali ya Taifa Muhimbili baada ya afya yake kuimarika na leo
ameruhusiwa kurudi nyumbani.
………………
Mgonjwa
Neema Wambura ambaye alikuwa akipatiwa matibabu katika Hospitali ya
Taifa Muhimbili (MNH) amemshukuru Rais John Pombe Magufuli baada ya afya
yake kuimarika na kuruhusiwa leo kurejea nyumbani.
Neema amemshukuru rais kwa kumwezesha kupata matibabu tangu alipofikishwa katika hospitali hiyo Februari 23, mwaka huu.
“Namuomba
Mwenyezi Mungu amuepushe Rais Magufuli na mambo mabaya yote. Sasa
nipata nguvu, nina furaha na naoga mwenyewe tofauti na awali,” amesema
Neema.
Pia, Neema amewashukuru madaktari na wauguzi wa Muhimbili kwa kumpatia huduma bora na kumwezesha kupona majeraha ya moto.
Neema
ambaye ni Mkazi wa Mkoa wa Mara alimwagiwa maji ya moto na mumewe
wakati alipokuwa akichemsha maji kwa ajili ya kupika ugali na kuungua
sehemu ya kifuani, shingo na mkono.
Mkuu
wa Idara ya Upasuaji na Daktari Bingwa wa Upasuaji, Dk Ibrahim Mkoma
amesema afya ya Neema inaendelea vizuri baada ya kufanyiwa upasuaji
sehemu ya shingoni ili kutenganisha shingo na sehemu ya kifua na kuziba
majera ya moto.
“Neema
anaendelea vizuri sasa anaweza kunyanyua shingo vizuri kabla ya hapo
alikuwa hawezi kuinyanyua wala kuizungusha,” amesema.
No comments :
Post a Comment