Mbunge wa Jimbo la Chalinze
Ridhiwani Kikwete (CCM) amesema Mradi wa Maji ambao ulitakiwa
kukabidhiwa mwezi huu jimboni humo umekwama.
Alisema hadi sasa hakuna matenki yaliyojengwa na pia mabomba hayajafukiwa hivyo mradi huo hauwezi kukamilika mwezi huu. Ridhiwani amesema vikao vya bunge vikianza anahitaji waziri mwenye dhamana kueleza fedha za maji zilizopelekwa Chalinze pia kujua mradi unaisha lini.
“Wananchi wangu wamechoka kusubiria maji ya matumaini wanahitaji maji nasio tena maneno hivyo bunge hili nitaomba waziri anipe majibu ya kueleweka “alisema Ridhiwani
No comments :
Post a Comment