Timu ya Manchester City imepigwa
faini ya paundi 35,000 na Chama cha Soka Uingereza (FA) kutokana na
tabia ya wachezaji wake katika mchezo ulioisha kwa sare ya 1-1 dhidi
ya Liverpool Machi 19.
Klabu hiyo imekiri kuonyesha utovu
wa nidhamu kwa kushindwa kuwadhibiti wachezaji wake kuonyesha tabia
nzuri uwanjani.
Uamuzi huo unatokana na tukio la
dakika ya 50, wakati refa Michael Oliver alipoipatia Liverpool
penati iliyofungwa na James Milner na kisha Sergio Aguero
alisawazisha goli.
No comments :
Post a Comment