Tuesday, March 28, 2017

MANCHESTER CITY YAPIGWA FAINI YA PAUNDI 35,000 NA FA

Timu ya Manchester City imepigwa faini ya paundi 35,000 na Chama cha Soka Uingereza (FA) kutokana na tabia ya wachezaji wake katika mchezo ulioisha kwa sare ya 1-1 dhidi ya Liverpool Machi 19.

Klabu hiyo imekiri kuonyesha utovu wa nidhamu kwa kushindwa kuwadhibiti wachezaji wake kuonyesha tabia nzuri uwanjani.

Uamuzi huo unatokana na tukio la dakika ya 50, wakati refa Michael Oliver alipoipatia Liverpool penati iliyofungwa na James Milner na kisha Sergio Aguero alisawazisha goli.

No comments :

Post a Comment