Washiriki
kutoka mikoa ya lindi,mtwara na Ruvuma wakiwamo maafisa Tehama
wakiendelea na mafunzo ya uanzishaji na uendelezaji wa tovuti katika
ofisi za umma ikiwemo halmashauri na ofisi za wakuu wa mikoa
…………..
Na Abdulaziz video,Mtwara
Katika kuelekea siku ya uzinduzi
huo ambao kwa kanda ya kusini utakaofanyika mkoani Mtwara Machi 27 mwaka
huu, wizara ya nchi ofisi ya Rais TAMISEMI kupitia mradi wa Uimarishaji
wa Mifumo ya Sekta za Umma Nchini PS3, imeendesha mafunzo kwa maafisa
habari wa ofisi za wakuu wa mikoa pamoja na halmashauri juu ya matumizi
ya tovuti, ambapo
miongoni mwawashiriki wameeleza kunufaika na mpango
huo utakaojenga utawala bora.
Wakizungumza na waandishi wa
habari baadhi ya washiriki wameshukuru Mradi wa PS 3 Kwa kuwezesha sekta
za umma kuwa na tovuti ambazo zitaanza kuwa hai ifikapo March 27 na
kusaidia maafisa habari kuanza kuwajibika ili jamii iweze habarika na
fursa mbali mbali bila gharama kubwa
Aidha walieleza kuwa Wakati
serikali ikielekea katika uzinduzi wa matumizi ya Tovuti katika ofisi za
umma ikiwa ni pamoja na ofisi za mikoa na halmashauri, Tayari baadhi ya
wananchi mkoani Mtwara wamepongeza hatua hiyo na kudai kuwa itasaidia
kuwapo kwa uwazi katika upatikanaji wa taarifa.
wananchi hao wamesema kutokana na
kuwapo kwa utandawazi unaochangiwa na kupanuka kwa teknolojia ya
mawasiliano, wananchi watanufaika na huduma hizo za Tovuti katika kupata
taarifa ambazo hazina ulazima wa kuzifuatilia katika makao makuu ya
ofisi husika.
Mafunzo hayo ambayo yameanza Machi
20 kwa kuhusisha maafisa habari na maafisa TEHAMA kutoka katika mikoa
ya Mtwara, lindi na Ruvuma yanatarajiwa kuhitimi
No comments :
Post a Comment