Na Masanja Mabula –Pemba ..
ZIARA za kushtukiza zinazofanywa na Mkuu wa Wilaya ya Wete Rashid Hadid Rashid bado zinaendelea na mara hii zimebaini madudu kwa wafanyabiashara ya vyakula katika Mji wa Wete .
Akiwa
eneo la Chasasa Mjini Wete ,Mkuu wa Wilaya amebaini mazingira machafu
ya biashara kwa muuza supu Suleiman Nassor (Ngamia ) ambaye amebainika
kutozingatia masharti yanayotakiwa kisheria .
Wafanyabiashara
wengine ambao Mkuu huyo wa Wilaya amewabainisha kwamba hawazingatii
usafi wa mazingira ni wauza maandazi , chipsi pamoja na wauzaji wa
vyakula kwenye migahawa
Akizungumza
katika eneo hilo Mkuu huyo wa Wilaya ambaye pia alikuwa amefuatana na
maofisa mbali mbali wa Serikali , ametoa muda wa siku moja kwa
mfanyabiashara huyo kuboresha mazingira ya biashara yake kinyume chake
atafungiwa kufanya biashara.
Amesema
mazingira ya biashara katika eneo hilo hayandani na sheria pamoja na
kanuni za afya , hivyo mfanyabiashara huyo anatakiwa kuhakikisha
mandhari ya eneo analouzia biashara yanaboreshwa na yakuwa safi ili
kulinda afya za walaji .
“Nakupa
muda wa siku moja uhakikishe mazingira katika eneo lako hili la
biashara unayaboresha , huwezi kuuza chakula (supu) katika sehemu
zilizochafu namna hii , baada ya siku moja maofisa wa afya watakuja
kuangalia na ikiwa hali bado ni hii tutakufungia ”alisema Mkuu wa Wilaya.
Aidha
Mkuu huyo wa Wilaya ametumia fursa hiyo kuwaasa wafanyabiashara na
wananchi wa Wilaya hiyo kila mmoja kuhakikisha anaweka safi mandhari inayomzunguka ili kujiepusha na magonjwa ya mripuko ikiwemo matumbo ya kuharisha na kipindupindu .
Naye Afisa wa Afya Wilaya hiyo Mwarabu Nuhu Mwarabu amewataka wananchi kuondoa kasumba kwamba usafi wa maziningira utafanywa na watendaji wa baraza la Mji pamoja na taasisi nyingine , bali wanapaswa kufahamu kamba maradhi yanapotokea hayachagui .
Amesema
Wilaya ya Wete imekuwa ikikumbwa na maradhi ya mripuko hususani
kipindupindu , na kuwatanabaisha kuchukua hatua za haraka na mapema
kuimarisha usafi ili kujiepusha na maradhi hayo ambayo yanachangiwa na
uchafu .
“Ni
jukumu la kila mmoja kuhakikisha maeneo yanayomzunguka anayaweka katika
hali ya kupendeza , na ondoeni kusumba ya kwamba usafi utafanywa na
baraza la Mji na taasisi za Serikali pekee kwani maradhi yanapotokea
hayachagui ”alisisitiza Mwarabu .
Mmoja
wa fanyabiashara Suleiman Juma Suleiman amewaomba wafanyabiashara
wenzake kushiriki katika usafi wa mazingira maeneo yao ya biashara ili
kufanya biashara zao ziweze kuwavutia wateja .
Ameeleza kwamba usafi sehemu za kazi ni
moja ya kivutio kwa wateja na kuwasisitiza wananchi kulifanya zoezi la
usafi ni la kudumu na kuacha kushuhulika wakati wa mvua tu kwani maradhi yanayotaka kuja hayasubiri msimu wa mvua .
No comments :
Post a Comment