Mwenyekiti na Katibu Mkuu wa
Sekta ya Uchukuzi, Dkt. Leonard Chamuriho (kushoto) akiongoza kikao cha
Baraza la Wafanyakazi wa sekta hiyo, kilichofanyika katika Ukumbi wa
Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Mkoani Dodoma leo.
Mwenyekiti na Katibu Mkuu wa
Sekta ya Uchukuzi, Dkt. Leonard Chamuriho (wa pili kulia) na wajumbe wa
Baraza la Wafanyakazi wa sekta hiyo wakiimba wimbo wa ‘Solidarity’ kabla
ya kuanza kikao cha taarifa ya utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2016/17
na mpango wa bajeti kwa mwaka 2017/18, kilichofanyika katika Ukumbi wa
Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Mkoani Dodoma leo.
Mkurugenzi wa Sera na Mipango
(Sekta ya Uchukuzi), Bw. Gabriel Migire akiwasilisha taarifa ya
utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2016/17 na mpango wa bajeti kwa mwaka
2017/18, kwenye Baraza la Wafanyakazi lilichofanyika katika Ukumbi wa
Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Mkoani Dodoma leo.
Sehemu ya wajumbe wa Baraza la
Wafanyakazi wa sekta ya Uchukuzi wakisikiliza taarifa ya utekelezaji wa
bajeti ya mwaka 2016/17 na mpango wa bajeti kwa mwaka 2017/18, kwenye
Baraza la Wafanyakazi lilichofanyika katika Ukumbi wa Idara ya
Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Mkoani Dodoma leo.
Picha na Biseko Lisso Ibrahim WUUM (T)
No comments :
Post a Comment