Wednesday, February 22, 2017

Zoezi la upasuaji kwa watoto wadogo muhimbili la malizika kwa mafanikio leo.


UP1
Kushoto ni Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Watoto, Profesa Zakaria Habib kutoka Falme za Kiarabu akiwa na timu ya  watalaam  wa Hospitali ya Taifa Muhimbili wakimuandaa mtoto mwenye umri wa miaka minane kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji wa hatua ya pili ya kushushwa kokwa kwenye korodani .
UP2
Madaktari wakifanya upasuaji wa njia ya matundu madogo kwa mtoto huyo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili  leo
UP3
Madaktari wakifanya upasuaji wa njia ya matundu madogo kwa mtoto huyo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili  leo
…………………………………………………
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) leo imehitimisha zoezi la  upasuaji mkubwa kwa njia ya matundu madogo kwa watoto ambao ulianza jumatatu wiki hii .
Upasuaji  huo umefanywa na Madaktari Bingwa wa Muhimbili waliobebea katika upasuaji wa
watoto kwa kushirikiana na mtaalam kutoka Hospitali ya King Faisal ya nchini Saudia Arabia Profesa Zakaria Habib .
Akizungumzia kuhusu upasuaji huo  Daktari Bingwa wa Upasuaji wa watoto wa Hospitali ya Taifa Muhimbili   Zaitun  Bokhary  amesema  upasuaji huo umekua na mafanikio makubwa na kwamba watoto wote waliofanyiwa upasuaji wanaendelea vizuri.
‘’ Tunamshukuru Mungu hadi leo tunapohitimisha zoezi hili watoto waliofanyiwa upasuaji huo  wanaendelea vizuri na  tayari wameanza kula pamoja na mazoezi ‘ ‘ amesema Dk. Bokhary.
Tangu kuanza kwa upasuaji huo Februari 20 mwaka huu kwa njia ya  matundu madogo ( Laparoscopy Surgery)  jumla ya watoto sita wamefanyiwa upasuaji huo.
Upasuaji huo umehusisha  upasuaji wa nyama iliyojitokeza katika sehemu ya haja kubwa kwa watoto, upasuaji wa kushusha kokwa katika korodani, upasuaji wa kushusha utumbo mkubwa na kutengeneza njia ya haja kubwa kwa watoto ambao wamezaliwa bila kuwa na njia ya haja kubwa, upasuaji wa kuondoa mfuko wa ziada kwenye koo kwa watoto na upasuaji kwa watoto wadogo ambao hawana celi mbalimbali na hivyo kushindwa kusukuma choo kwenye utumbo mkubwa

No comments :

Post a Comment