Mlezi wa shirikisho la wanaafunzi
wa vyuo vikuu (CCM)mkoani Pwani,,alhaj Abdul Sharif,akifunga mkutano
ulioandaliwa na shirikisho hilo,kwa ajili ya kuchagua viongozi nafasi ya
katibu,mwenezi na mhamasishaji..(Picha na Mwamvua Mwinyi)
BAADHI ya wanachama wa shirikisho
la wanafunzi wa vyuo vikuu la Chama Cha Mapinduzi (CCM)mkoani Pwani
wakipiga kura kuchagua viongozi wa nafasi zilizoachwa wazi ikiwa ni
pamoja na katibu,mhamasishaji na mwenezi.(Picha na Mwamvua Mwinyi)
BAADHI ya wanachama wa shirikisho
la wanafunzi wa vyuo vikuu la Chama Cha Mapinduzi (CCM)mkoani Pwani
wakifuatilia mkutano wa uchaguzi uliofanyia kwa lengo la kuchagua
viongozi wa nafasi zilizoachwa wazi ikiwa ni pamoja na
katibu,mhamasishaji na mwenezi.(Picha na Mwamvua Mwinyi)
…………………………………………………………………………
Na Mwamvua Mwinyi,Bagamoyo
SHIRIKISHO la Wanafunzi wa Vyuo
Vikuu Tanzania (TAHLISO) la Chama Cha Mapinduzi limetakiwa kuwa moja ya
mabalozi wa chama na serikali yake kwa kusema yale
yanayotekelezwa na
Rais dk.John Magufuli na watendaji wake.
Aidha wasomi hao wametakiwa kuwa
wazalendo wa nchi yao ikiwa ni pamoja na kuacha kutumika kama ngazi ya
kupandisha watu wachache kwa maslahi yao.
Hayo yalisemwa Bagamoyo na mlezi
wa tahliso,mkoani Pwani,alhaj Abdul Sharifu wakati wa uchaguzi wa kujaza
nafasi za baadhi ya viongozi wa shirikisho hilo kimkoa.
Alhaj Sharifu alisema ,shirikisho
hilo ni nguzo pekee ndani ya chama ambayo inapaswa kutia nguvu katika
kukisemea na serikali yake iliyopo madarakani.
Alieleza kwamba,awamu ya nne
,iliona mbali na kuanza kushirikisha wanafunzi wa vyuo vikuu kujiunga
kwenye chama hivyo watumie mwanya huo kueleza na mazuri yanayofanywa
pasipo kuwa nyuma.
Alhaj Sharif alisema ,lengo kuu
la chama ni mashirikisho hayo kupikwa kisiasa na kuwa viongozi wenye
maadili mema baadae na kuwa viongozi bora na si bora kiongozi.
Katika hatua nyingine,alhaj
Sharif alisema kuna baadhi ya watu wamekuwa wakilalamika hali ya
kiuchumi ni mbaya na kusababisha wananchi kuwa kwenye hali ngumu ya
kimaisha.
“Serikali inatambua nini
inakifanya,na kudhibiti madudu yaliyokuwa yakifanyika,hivyo wasomi kwa
kuwa ni waelewa jaribuni kuwaelewesha wananchi juu hili”alisema.
Alhaj Sharifu ambaye pia ni
mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi (CCM) wilaya ya Bagamoyo alisema rais dk
Magufuli amefanikisha suala zima la kodi kukusanywa
kikamilifu,kuwadhibiti walaji wa fedha za serikali na kuwabana watu
waliokuwa wakikwepa kodi .
Alifafanua,hali hiyo ilikuwa
ikisababishia nchi hasara kubwa kwa kuikosesha mapato ya ndani ambapo
kwasasa kila mmoja anajionea mapato ya serikali yanainuka.
“Nyie ni wasomi na viongozi wa siasa baadae ,waelezeni wananchi faida na malengo ya miaka ijayo “alisema alhaj Sharif.
Aliwataka viongozi waliochaguliwa kuweka mikakati ya kuwapa mafunzo ya itikadi kwa wanachama wao ili waweze kukijua chama na kuiva kisiasa.
Aliwataka viongozi waliochaguliwa kuweka mikakati ya kuwapa mafunzo ya itikadi kwa wanachama wao ili waweze kukijua chama na kuiva kisiasa.
Kwa upande wake mwenyekiti wa
shirikisho hilo Filemon Mabuga alisema shirikisho limekuwa msaada mkubwa
kwa chama na hata kwenye uchaguzi mkuu uliopita wa 2015 walifanya kazi
kubwa ya kukipa chama ushindi .
Katika uchaguzi huo Method Mselewa amechaguliwa kuwa katibu wa
shirikisho hilo mkoani Pwani na nafasi ya mhamasishaji alipata Magina
huku na nafasi ya mwenezi ameshinda Salum Kiguni.
No comments :
Post a Comment