Monday, February 13, 2017

MGOMBEA WA KITONGOJI CHA MAGOMENI B AAHIDI MAENDELEO


VUMA 2
DIWANI wa kata ya Magomeni ,wilayani Bagamoyo,Mwanaharusi Jarhuf,akimnadi mgombea wa kitongoji cha Magomeni B,Rajab Swedy katika mkutano wa kampeni uliofanyika eneo la Bagabest.
VUMA 1
Meneja wa kampeni wa uchaguzi mdogo kitongoji cha Magomeni B,Kata ya Nianjema,Bagamoyo,alhaj Abdul Sharif,akiwa amepokea kadi kutoka kwa wanachama wa CUF walioamua kurejea CCM,katika mkutano wa kampeni ulifanyika Kidongo Chekundu-Bagabest ambapo wanachama Zaidi ya 30 kutoka CUF walirejea CCM.(Picha na Mwamvua
Mwinyi)
………..
Na Mwamvua Mwinyi,Bagamoyo
MGOMBEA wa nafasi ya mwenyekiti wa kitongoji cha Magomeni B,wilayani Bagamoyo, kupitia CCM,Rajabu Swedy ameahidi kusimamia kero ya ukosefu wa umeme,maji na miundombinu ya barabara katika maeneo yenye changamoto hiyo.
Amesema endapo atapewa ridhaa na wananchi siku ya februari 19 mwaka huu,atahakikisha anavalia njuga suala zima la maendeleo kwa kushirikiana na serikali na wananchi.
 
Aliyasema hayo kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika Kijiwe Poa,Bagabest na Chemchem Kidongo Chekundu.
Swedy alisema anatambua kero mbalimbali sugu zinazowasumbua wananchi hao hivyo atajituma kwa ari na mali kuzitatua.
Alisema hagombei nafasi hiyo kwa sifa ama maslahi binafsi bali ni kuleta maendeleo ili kupiga hatua kutoka walipo sasa.
“Malengo yangu ni kukabili changamoto zilizopo kwa wananchi ikiwa ni pamoja na masuala ya miundombinu, mikopo,maji,nishati ya umeme, afya na elimu ambayo atayapa kipaumbele katika kuyapeleka halmashauri”
“Tutakwenda kwa vipaumbele kama nyie mtakavyo pendekeza kwani lazima tuwe na malengo ya utatuzi wa changamoto hizi ” alisema Swedy.
Kwa upande wake meneja wa kampeni ya uchaguzi mdogo kitongoji cha Magomeni B,alhaj Abdul Sharif,alipokea kadi zaidi ya 30 kutoka kwa wanachama wa CUF ambao wamerejea CCM.
Alisema wanachama hao kurudi CCM inaashiria uchaguzi huo mdogo unatarajiwa kufanyika februari 19 CCM kushinda kwa kishindo.
Sharif aliwaomba wananchi wamchague Swedy na kuachana na wapinzani kwani CCM inatekeleza kwa yale inayoyaahidi.
Sharif alisema Swedy anajiuza kwa sera na ilani ya chama chake na jimbo la Bagamoyo kuwa na madiwani wote wa CCM ,hivyo atasaidia kuungana pamoja nao kutatua kero hizo kirahisi.
Nae mwenyekiti wa halmashauri ya Bagamoyo Ally Ally Issa,alisema halamshauri hiyo imetenga kiasi cha sh.mil 50 kwa ajili ya kujenga miundombinu kwenye kata ya Nianjema.
Mwenyekiti huyo amabe pia ni diwani wa kata ya Fukayose ,alifafanua kwamba,fedha hizo zinafikia na kitongoji cha Magomeni B kujenga na kuboresha miundombinu yake ya barabara mbovu.
Ally aliwataka wana Magomeni B,kuacha kufanya makosa ,kuchagua vyama vya upinzani,wasibet katika uchaguzi huo,bali wamchague RAjabu Swedy

No comments :

Post a Comment