Sunday, February 5, 2017

Breaking News!! AJALI YAUA WATU ZAIDI YA WATATU MOSHI,YUMO MWANDISHI WA HABARI NA MWENYEKITI WA CCM


ajali ccm
Habari tulizozipata hivi punde kutoka mkoani Kilimanjaro zinasema kuwa watu zaidi ya watatu wamefariki dunia akiwemo mwandishi wa habari wa gazeti la Habarileo Anord Swai na mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Hai katika ajali ya gari dogo.
Ajali imetokea maeneo ya Mwika Mawanjeni maarufu kama Bar Mpya Moshi mkoani Kilimanjaro.
Inaelezwa kuwa ndani ya gari walikuwemo watu sita wakiwemo viongozi wa CCM wakitoka kushiriki sherehe za miaka 40 ya CCM kimkoa yaliyofanyika katika ukumbi wa shule ya Msingi Shauri Tanga wilayani Rombo.
Chanzo cha ajali inaelezwa kuwa ni fuso kufeli breki na kuligonga gari dogo.
“Waliofariki ni mwenyekiti wa Uvccm wilayani hai na mwandishi wa habari Leo Arnold Swai, mjumbe wa NEC ya CCM na Katibu wa CWT mkoa wa Kilimanjaro ally Mmbaga na wanafunzi makada wa CCM kutoka vyuo vikuu vya ushirika na KCM. Majeruhi wa ajali hiyo ni Jackson Kimambo amekimbizwa Hospitali na wote walikuwa wakitoka kwenye maadhimisho ya kilele cha miaka 40 ya kuzaliwa CCM wilayani Rombo” -Ujumbe wa mwandishi wa habari Lucy Ulomi ambaye sasa yupo hospitali ya KCMC akifuatilia habari hiyo.

CHANZO MALUNDE1BLOG

No comments :

Post a Comment