Friday, December 16, 2016

PROF. MBARAWA ATOA MAAGIZO KWA WAKUU WA WILAYA


prof
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akizungumza na wakazi wa kijiji cha Kisorya Wilayani Bunda, mkoani Mara wakati alipotembelea na kukagua kivuko cha MV Ujenzi kinachotoa huduma kati ya Rugenzi Ukerewe na Kisorya wilayani hapo.
prof-1                                            
Mbunge wa Mwibara Mhe. Kange Rugora (wa pili kushoto), akiongea na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (wa pili kulia), katika ziara yake mkoani Mara wakati alipotembelea na kukagua kivuko cha MV Ujenzi kinachotoa huduma kati ya Rugenzi Ukerewe na Kisorya kilichopo Wilaya ya Bunda.
prof-2
Meneja wa Wakala wa Ufundi na Umeme Nchini (TEMESA), Eng. Fredinand Mishamo akitoa maelezo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa wakati alipotembelea na kukagua kivuko cha MV Ujenzi kinachotoa huduma kati ya Rugenzi Ukerewe na Kisorya wilayani hapo.
prof-3
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, akishuka kutoka katika kivuko cha MV Ujenzi kinachotoa huduma kati ya Rugenzi Ukerewe na Kisorya wilayani Bunda, wakati alipotembelea na kukagua kivuko hicho.
prof-4
Muonekano wa kivuko cha MV Ujenzi kinachotoa huduma kati ya Kijiji cha Rugenzi Ukerewe na Kisorya wilayani Bunda.
prof-5
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, akikagua kivuko cha MV Mara kinachotoa huduma kati ya Kijiji cha Mugara na Kuruge wilayani Bunda, wakati alipotembelea na kukagua kivuko hicho. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Mwl. Lydia Bupilipili.

kero
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, akisikiliza kero kutoka kwa mmoja wa wananchi wa Kijiji cha Iramba, Wilaya ya Bunda, mara baada ya kukagua kivuko cha MV Mara na kuongea na wananchi hao.
athari
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, akiangalia athari za miundombinu ya barabara kwenye Daraja la Burendabufwe lilibomoka kutokana na mvua zilizonyesha hivi karibuni katika barabara ya Kibara-Iramba wilayani Bunda.
prof-6
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, akicheza nyimbo za asili za kabila la wakerewe, wilaya ya Bunda kabla ya kuongea na wakazi wa kijiji cha Iramba, mkoani Mara.
prof-7

Mbunge wa jimbo la Mwibara, Mhe. Kange Lugora (kushoto) akiteta jambo na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (kulia), wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Mwibara.
………………….

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa amewaagiza Wakuu wa Wilaya  na Wakurugenzi wa Halmashauri kote  nchini

kuhakikisha wanafuatilia na kusimamia kwa ukaribu utekelezaji
wa miradi mbalimbali  inayotekelezwa kwa kutumia Mfuko wa Barabara katika maeneo yao.
Akizungumza Wilayani Bunda, mkoani Mara baada ya kupokea taarifa ya hali ya miundombinu Wilayani hapo, Waziri Prof. Mbarawa amesema kuwa hatua hiyo pia itasaidia kudhibiti upotevu wa fedha za wananchi pamoja na kuongeza kasi ya utekelezaji wa miradi hiyo.
“Nawaagiza Wakuu wa Wilaya wote na Watendaji wa Halmashauri kuhakikisha wanasimamia ipasavyo miradi inayotekelezwa kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara ambazo ni fedha za wananchi”, ameagiza Prof. Mbarawa.
Aidha, amemhakikishia Mkuu wa Wilaya ya Bunda kuwa Serikali itaendea kufanya kila linalowezekana kuimarisha miundombinu kwa maendeleo ya watanzania.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya hiyo Mwl.Lydia Bupilipili, amesema kuwa wilaya hiyo imejiwekea utaratibu  wa kufuatilia miradi hiyo lakini pia inawaelimisha watendaji kata na vijiji kuhusiana na sheria ya barabara.
Katika hatua nyingine, Waziri Mbarawa ametembelea Kivuko cha Mv Mara na Mv Ujenzi na kuahidi kuboresha utoaji wa huduma katika vivuko hivyo ikiwemo ujenzi wa jengo la abiria katika kijiji cha Iramba na Kisorya.
Amewasisitiza kudhibiti mapato yatokanayo na vivuko hivyo ili kuweza kuongeza ufanisi na utendaji wa vivuko hivyo.
Naye, Meneja wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA), Mkoani Mara amemhakikishia Waziri huyo kufunga mifumo ya kielektroniki ili kudhibiti mianya ya upotevu wa mapato.
Aidha, Waziri Prof. Mbarawa ametembelea barabara ya Busambala – Kisorya (KM 120), na kutoridhishwa na hatua ya ujenzi wake, hivyo kutoa miezi sita kwa Mkandarasi wa Kampuni ya ujenzi ya Nyanza Roads Works anayejenga barabara hiyo kukamilisha ujenzi wake.
Prof. Mbarawa ameanza ziara yake ya siku mbili mkoani Mara ambapo anatarajia kukagua miradi mbalimbali inayotekelezwa na Wizara yake.
Imetolewa na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, kitengo cha Mawasiliano Serikalini

No comments :

Post a Comment