Monday, December 19, 2016

Mwanzilishi wa JamiiForums Aachiliwa kwa Dhamana, Kesi Yake Kuunguruma Desemba 29


mkurugenzi-wa-jamii-forums-maxence-melo-1PICHA KWA HISANI YA https://globalpublishers.co.tz
DAR ES SALAAM: Mkurugenzi wa Jamii Media Limited na Mwanzilishi wa Mtandao wa JamiiForums, Maxence Melo, leo Desemba 19, 2016 ameachiliwa kwa dhamana na Mahakama Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam baada ya kukaa lupango kwa takribani siku 7.
mkurugenzi-wa-jamii-forums-maxence-melo-2Mkurugenzi wa Jamii Media Limited, Maxence Melo akifikishwa mahakamani.
Melo ambaye anakabiliwa na mashtaka matatu likiwemo la kuendesha tovuti ambayo haijasajiliwa nchini, amedhaminiwa na wadhamini wawili ambao ni Judith Kapinga na Kiiya Joel Kiiya, wote wawili wametakiwa kuweka bondi ya Tsh. Milioni 5 kila mmoja ili wamdhamini jambo amabalo wametekeleza.
mkurugenzi-wa-jamii-forums-maxence-melo-3Mbali kuweka bondi hiyo, wadhamini hao pia walitakiwa kuambatanisha na kuacha mahakamani hapo barua za utambulisho wa kazi na mahali wanapofanyia kazi jambo ambalo pia walitekeleza.
mkurugenzi-wa-jamii-forums-maxence-melo-4Akiwana mawakili wke nje ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya kuachiliwa kwa dhamana.
Baada ya kupata dhamana, kesi hiyo Melo itatajwa tena Desemba 29 mwaka huu.
mkurugenzi-wa-jamii-forums-maxence-melo-6Melo akizungumza na wanahabari kwenye Ukumbi wa Hoteli ya Serena, Dar.
Baada ya kuachiwa kwa dhamana, Melo aliitisha mkutano na waandishi wa habari katika Hoteli ya Serena, Posta jijini hapa ambapo mbali na mambo mengine, amewashukuru waandishi wa habari kwa jinsi walivyokuwa wakiripoti suala la kesi yake, na kuwataka wasiogope kutoa taarifa au kuwasilisha mawazo yao kwenye vyombo vya habari na kuongeza kuwa hatakuwa na mengi ya kuzungumza kwa sababu tayari suala hilo lipo mahakamani.

No comments :

Post a Comment